Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya simu ya Airtel itachezesha droo
ya kwanza ya mwenzi ya promosheni ya Shinda Nyumba na Airtel Yatosha leo ili
kumtafuta mshindi wa nyumba ya kisasa iliyoko Kigamboni jijini Dar es Salaam
.Akizungumza
kuhusu droo hiyo Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando, alisema Airtel
kupitia promosheni ya Airtel yatosha inaendelea kuwazawadia wateja zawadi
mbalimbali ikiwemo pesa taslimu kiasi cha sh. milioni moja kila siku.
Aliongeza kuwa
zaidi ya wateja 21 wamejishindia kiasi cha zaidi ya sh. milioni 21 na bado kuna
nafasi kwa wateja zaidi ya 69 kuondoka na kitita cha kiasi hicho kila siku.
Meneja huyo
aliendelea kusema kuwa mbali na zawadi ya sh. milioni moja, Airtel pia inatoa
zawadi ya kila mwezi kwa mshindi ambapo nyumba tatu za kisasa zimejengwa na
Shirika la Nyumba la Taifa NHC maeneo ya Kigambopni jijini Dar es Salaam.
"Natoa
mwito kwa wateja ambao bado hawajajiunga huduma ya Airtel yatosha kujiunga kwa
kununua kifurushi cha wiki, siku au mwezi na kuunganishwa moja kwa moja kwenye
promosheni na kupata nafasi ya kuingia kwenye droo ya kuibuka mshindi wa nyumba
au fedha kila siku," alisema Jackson.
Kwa upande wake
Ofisa Habari wa Shirka la Nyumba la NHC, Yahaya Charahani, alisema nyumba
zimekamilika na zipo tayari kukabidhiwa kwa washindi. "Tunaamini mshindi
atakayepatikana atafurahia mandhari mazuri, mazingira na nyumba yenye ubora wa
kiwango cha juu.
Nachukua nafasi hii kuwahimiza Watanzania wapate muda
wa kutembelea nyumba hizi ili nao wapate nafasi ya kuona miradi mbalimbali
tuliyonayo," alisema
No comments:
Post a Comment