15 August 2013

WANANCHI WAKOSA MAJI MIAKA KUMI



Na Esther Macha, Mbeya
WANANCHI wa Kata ya Mshewe Kijiji cha Njelenje Wilaya ya Mbeya wamelalamikia kukosekana kwa maji kwa muda wa miaka 10 licha ya uongozi wa kata hiyo kuendelea kuwachangisha michango ya mabomba wananchi hao

Walisema ni jambo la kusikitisha kuona uongozi uliopo unafanya kazi ya kuchangisha michango tangu mwaka 2009 mpaka sasa na dalili za kuwepo maji hakuna na hata kusomewa mapato na matumizi ya fedha hizo hayapo.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kwa kushirikiana na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) umebaini kuwa maji ambayo wanatumia wananchi wa kijiji hicho ni yale ambayo yanatoka kwenye chanzo ambacho ni makaburi ya watu ambayo hata hivvyo hayana usalama wowote ambapo gazeti hili lilibaini kuwa maji hayo ambayo yapo kwenye chemchem.
Mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Njelenje, Rashid Odati alisema kuwa toka wameanza kuchangia maji ni muda mrefu, kwani maji yaliyopo ambayo wanatumia ni hatari kwa afya za wananchi kutokana na maji wanayotumia kutoka kwenye chanzo ambacho kipo karibu na vyoo na makaburi ya watu.
"Hapa tulipo hatuelewi hatma yetu ni nini kwani maji tunayotumia ni hatari sana kwa afya zetu hebu ndugu mwandishi wa habari angalia hicho chanzo kipo kati kati ya makaburi kwa hali hii sidhani kama kuna uhakika wa sisi wananchi kupata maradhi," alisema mkazi huyo.
Akizungumzia kuhusu viongozi alisema wamekuwa na sababu nyingi za kutoa kwa wananchi ambazo hazina umuhimu wowote kutoka kwa wananchi kwani fedha ambazo zinachangwa na zimekuwa kama mtaji kwao wa kuendeshea maisha yao.
"Mfano huyu diwani wetu† amekuwa na amri zake kwa wananchi kwa kutumia cheo chake kukandamiza wananchi , sisi hatutaki diwani awe mwiba kwetu kwa kutumia† nafasi yake kama fimbo kwa wananchi," alisema Odati.
Mkazi mwingine, Teddy Mwakaje alisema kutokana na shida ya maji hakuna maendeleo yeyote ambayo wanafanya kutokana na muda mwingi kutumia kutafuta maji kwani hata yaliyopo kwenye chazo nayoi bado ni tatizo kuyapata licha ya kutokuwa na usalama wa kutosha.
Akizungumzia tatizo hilo la maji Mwenyekiti wa kitongoji cha Kizota, John Kapange alisema kuwa kero hiyo ya maji ni ya muda mrefu katika kijiji hicho na kusababisha wananchi kutoka usiku wa manane kwenda kutafuta maji kwenye visima.
Akijibu malalamiko hayo ya wananchi Diwani wa Kata ya Mshewe, Fabian Mwakasole alisema tatizo hilo la maji katika Kijiji cha Njelenje ni la muda mrefu na kwamba toka anaingia madarakani mwaka 2010 amelikuta.


No comments:

Post a Comment