15 August 2013

WATUMIA MIFUKO YA RAMBO BADALA YA KONDOMU



 Na Florah Temba, Moshi
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida baadhi ya wananchi mk o a n i Ki l ima n j a r o , wamelazimika kutumia mifuko ya plastiki (malboro) kujikinga na maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwi, huku wengine wakichangia kondomu, jambo ambalo ni hatari na linaelezewa kuwa moja ya chanzo cha ongezeko la maambukizo mapya ya ugonjwa huo mkoani humo
. Takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwikatika Mkoa wa Kilimanjaro, kimepanda kutoka asilimia 1.9 mwaka 2007/2008 hadi kufikia asilimia 3.8 mwaka 2011/2012.
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika lisilokuwa la kiserikali, linalojihusisha na mapambano dhidi ya Ukimwimkoani Kilimanjaro (KACA) Faraji Swai alisema wananchi wa maeneo ya vijijini wako hatarini zaidi kupata maambukizo ya ugonjwa ya ukimwikutokana na kwamba wengi bado hawajafikiwa.
Alisema Shirika la Kacakatika utoaji elimu ya mapambano dhidi ya Ukimwikwa jamii, wamefika katika baadhi ya vijiji mkoani Kilimanjaro na kuwakuta wananchi wakitumia mifuko ya plastiki (malboro) kama kinga ya kujikinga na maambukizo ya Ukimwihuku wengine wakichangia kondomu jambo ambalo liliwashangaza.
Alisema vijiji ambavyo walikuta wananchi wakitumia malboro kujikinga na Ukimwina kuchangia kondomu ni pamoja na Kahe, Mikocheni, Newland na TPC vyote vya Wilaya ya Moshi, huku baadhi ya mitaa katika Kata ya Njoro Manispaa ya Moshi wakikutwa nao wakichangia kondomu moja zaidi ya mtu mmoja.
"Ni jambo la kushangaza kwani yapo maeneo katika Mkoa huu wa Kilimanjaro ambayo tumefika kutoa elimu ya kujikinga na maambukizo ya Ukimwina wananchi kutueleza kuwa wao hutumia malboro kama kondomu kujikinga na ugonjwa huo huku wengine wakifua kondomu mara baada ya kutumia ili kutumia tena wakati mwingine au kumpa mwenzake naye ajikinge, kwa kweli hii ni hatari sana," alisema Swai.
Alisema maeneo ya mjini kondomu zimekuwa zikizagaa kwa kukosa watumiaji lakini yapo maeneo ya vijijini yenye uhitaji mkubwa na hayajafikiwa jambo ambalo limesababisha kasi ya ukimwikatika maeneo hayo kuzidi kukua.
Alisema maeneo mengine ambayo yameonekana kuwa na kasi ya maambukizo ya Ukimwina yanauhitaji mkubwa wa kondomu ni Kibosho, Mwika na Marangu Mtoni hivyo kunahitajika jitihada za makusudi za kuwanusuru wananchi wa maeneo hayo.
Swai aliongeza kuwa zipo sababu nyingi ambazo zinachangia kasi ya maambukizo mapya ya Ukimwiambapo ni pamoja na umaskini wa kupindukia ambao huwafanya wasichana wengi hususan wa vyuo vikuu kujiingiza kwenye biashara ya kuuza miili.
Alisema sababu nyingine ni baadhi ya watu ambao wameshajitambua kupata maambukizo ya Ukimwikuueneza kwa makusudi, ulevi wa kupindukia, matumizi ya dawa za kulevya pamoja na vijana wengi kutokuwa na kazi za kufanya na hivyo kujiingiza kwenye biashara za ngono.
"Kwa sasa wananchi wengi hawaogopi tena Ukimwi, wanaona ni hali ya kawaida lakini sisi kama shirika tumekuwa tukijitahidi kutoa elimu hasa kwa vijana kwani kama hatutakuwa makini tutaipoteza nguvu kazi ya taifa hapo baadaye," alisema.
"Sheria ya Ukimwiinasema mtu ambaye atabainika kuambukiza ugonjwa huo kwa makusudi ashtakiwe, sasa tunaomba ifanye kazi na Serikali iweke mkazo katika hili, ihakikishe wale wote watakaobainika kukiuka sheria hii wanachukuliwa hatua kali za kisheria," alisema.
Hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, akizungumzia ongezeko la maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwikwa mkoa huo, alisema imeonekana kupanda mara dufu, hivyo kuwataka wananchi mkoani humo kubadili tabia na kuepuka ngono zembe.

No comments:

Post a Comment