15 August 2013

MALARIA YAENDELEA KUITESA MARA



Na Veronica Modest, Musoma
MOJA ya changamoto inayosababisha Mkoa wa Mara kuendelea kuwa kinara sugu wa ugonjwa wa malaria ni kutokana na wananchi kuwa na imani potofu juu ya matumizi ya dawa za malaria pamoja na matumizi mabaya ya vyandarua wakati wa kulala.

Wakichangia hoja ya namna ya kudhibiti ugonjwa huo katika Mkoa wa Mara juzi katika kikao cha wadau wa malaria wadau hao walisema kuwa kuna kila sababu ya kutafuta njia sahihi ya kupambana na ugonjwa huo kwani Mkoa wa Mara umeonekana kuwa tatizo kubwa.
Akiwasilisha mada yake mbele ya wadau hao Mratibu wa kampeni ya unyunyiziaji wa dawa ya kutoka nyumbani, Yusufu Mwita alisema kuwa mkoa umezidi kuwa kinara wa ugonjwa huo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa kutokana na wananchi kuwa na imani potofu juu ya dawa za malaria pamoja na elimu duni.
Alizitaja sababu za mikoa mingine kufanikisha kampeni hiyo kuwa ni pamoja na mwitikio mzuri wa matumizi mazuri ya tiba sahihi ya dawa za malaria,matumizi ya vyandarua wakati wa kulala na ushirikiano mzuri wa wananchi katika zoezi zima la unyunyiziaji wa dawa ya ukoka majumbani.
Mwita alisema kuwa Mkoa wa Mara unaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizo ya ugonjwa huo kwa asilimia 25.6 mwaka 2012 na asilimia 30.5 kutoka mwaka 2007 huku Mkoa wa Kagera ukipunguza maambukizo hayo kwa asilimia 8.5 mwaka 2012 na asilimia 41.2 kutoka mwaka 2007.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa alisema kuwa licha ya juhudi mbalimbali za wadau na taasisi mbalimbali kujitokeza katika kupambana na ugonjwa wa malaria lakini juhudi hizo hazionekani kuleta maendeleo kama mikoa mingine inavyoleta mabadiliko katika kupunguza tatizo hilo.
Tuppa alisema kuwa umefika wakati sasa malaria itangazwe kuwa ni tatizo kwa mkoa wa Mara hivyo liboreshwe kwa kila wilaya kukaa na kujadili ili kuhakikisha wanatoka na mpango mkakati wa kupambana na ugonjwa wa malaria.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tarime, John Henjewelle alisema kuwa moja ya mambo yanayosababisha ugonjwa huo kuendelea kuwa sugu katika mkoa wa Mara ni pamoja na uchafu kwa kuwa watu waliowengi hawazingatii suala la usafi wa mazingira katika maeneo yanayozunguka makazi yao.
Aidha Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Elias Goroi alisema kuwa ili kufanikisha kazi hiyo ni lazima ushirikishwaji wa wadau pamoja na wahusika wa maeneo uwepo katika kutoa elimu kwa wananchi wa maeneo husika hali ambayo itasaidia katika kumwondoa hofu mwananchi wa kawaida na hivyo kazi hiyo kukamili

No comments:

Post a Comment