Esther Macha, Mbeya na Said Hauni,
Lindi
WAKATI Sikukuu
ya Wakulima ya Nanenane ikiwa imekaribia kufikia kileleni, kumeibuka mgongano
baina ya Chama cha Wakulima (TASO) na Serikali kuhusu siku ya kufanyika kwa
maadhimisho hayo kati Agosti 7 na 8, mwaka huu
.Mgongano huo
umekuja baada ya Serikali kutaka maadhimisho hayo yafanyike Agosti 7, mwaka huu
TASO kikiweka msimamo wake wa kusherehekea maadhimisho hayo Agosti 8, mwaka
huu.
Kauli hiyo
imetolewa jana na Mwenyekiti wa TASO, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Kapteni
Mstaafu Noel Nkoswe, wakati wa mkutano wa majumuisho na waandishi wa habari
baada ya kuibuka vuta nikuvute na serikali kuhusu kilele cha maadhimisho hayo
ya wakulima.
Kapteni Nkoswe,
alisema wao kama chama cha wakulima msimamo wao upo pale pale, ni sherehe hizo
zifanyike Agosti 8, mwaka huu kama ilivyopangwa kila mwaka.
"Wa k u l
ima we t u l a z ima washerehekee sikukuu yao kama kawaida mpango wa
kubadilisha siku haupo kabisa. TASA tunafanya maadhimisho Agosti 8 na zawadi za
wakulima tutatoa siku hiyo hiyo na wao kama serikali watafanya kiserikali kama
kawaida, sisi upande wetu sikukuu yetu ni Agosti 8," alisisitiza.
Kwa upande wake
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma, alisema wamepokea barua ya
Serikali inayotaarifu kilele cha Nanenane ni Agosti 7, mwaka huu kutokana na
Sikukuu ya Idd kuaangukia Agosti 8, mwaka huu.
"Sisi
serikali tunafanya maadhimisho haya Agosti 7 mwaka huu kama barua ya serikali
ilivyoagiza kuwa kilele hicho kifanyike," alisema.
Wakati huo huo,
wakulima Kanda ya Kusini, inayojumuisha mikoa ya Lindi na Mtwara, wametakiwa
kuacha tabia ya kilimo cha mazoea, badala yake wakigeuze kuwa cha kibiashara
kwa kuzalisha zaidi mazao yanayolenga mahitaji halisi ya walaji.
Rai hiyo
ilitolewa jana na Mwenyekiti wa TASO Kanda ya Mtwara, Menas Likuku, alipokuwa
akisoma risala, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Sikukuu ya Wakulima
Nanenane,yanayofanyika viwanja vya Ngongo, Manispaa ya Lindi.
Akisoma risala hiyo mbele ya mgeni
rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Joseph Simbakalia, mwenyekiti huyo wa TASA
alisisitiza wananchi kuzalisha mazao kwa malengo ya kibiashara na kuangalia
fursa za masoko yaliyopo.
Likuku alisema TASA kanda ya kusini
inawahamasisha wakulima wa Mikoa ya Lindi na Mtwara, kutumia fursa za kiuchumi
zilizopo kwa lengo la kukuza ustawi wa jamii kupitia uzalishaji wa mazao ya
kilimo, mifugo na sekta nyingine.
Alizitaja sekta hizo kuwa ni pamoja
na uvuvi, urinaji wa asali, viwanda vidogo vidogo vya usindikaji wa mazao ya
kilimo na mifugo kwa kulenga masoko yaliyopo na yale yanayotarajiwa kuwepo
kutokana na kukua kwa sekta ya gesi.
Mwenyekiti huyo alisema tangu kuanzishwa kwa maonesho
ya hayo miaka 10 iliyopita, kumekuwa na mafanikio mbalimbali ikiwa ni pamoja
kukamilika kwa upimaji wa viwanja (50) vya eneo la ndani ya kwa ajili ya wadau.
No comments:
Post a Comment