Na Mwandishi Wetu
WAHAMIAJI haramu
8,509 kutoka nchi za Rwanda,
Burundi na Uganda, wameondoka nchini kwa hiari yao baada ya agizo la
Rais Jakaya Kikwete, ambalo alilitoa hivi karibuni akiwa ziarani mkoani Kagera.Wahamiaji
hao, wametoka katika Mikoa ya Kagera, Geita na Kigoma ambapo taarifa
iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, ilisema kati ya wahamiaji hao, 5,521 wamerudi nchini Rwanda, Burundi
2,744 na Uganda
244.
Katika
operesheni hiyo, silaha 60 zimerejeshwa kwa hiari zikiwemo bunduki aina ya SMG
na magobole ambapo taarifa hiyo iliongeza kuwa, operesheni ya kuwarejesha
wahamiaji hao pia imehusisha urejeshaji wa mali na mizigo.Vitu
vingine vilivyorejeshwa ni mifugo 1,996 katika nchi hizo. Kurejea kwa wahamiaji
hao ni utekelezaji wa agizo la Rais Kikwete ambaye alitoa siku 14 wawe
wameondoka nchini kwa hiari yao
ndani ya kipindi hicho.
"Serikali
imefurahishwa sana na ushirikiano tuliopata
kutoka nchi za Rwanda, Burundi na Uganda hasa za kuwapokea hawa
wahamiaji wakishirikiana na nchi yetu katika kazi hii."Tunawaomba wahamiaji wengine ambao bado
wako nchini, waondoke haraka iwezekanavyo kabla hatua ya kuwaondoa kwa nguvu
hazijaanza," iliongeza taarifa hiyo
No comments:
Post a Comment