NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI), Aggrey Mwanri amemtaka Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Benedict Ole
Kuyan apeleke timu ya wakaguzi wilayani Kilindi kwenda kuchunguza fedha
zilizopelekwa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Jaila
.Agizo hilo alilitoa baada ya kuonekana hakuna uwiano wa fedha zilizotumika
na kazi iliyofanyika.Mwanri aliyasema hayo juzi baada ya kufika kwenye kituo hicho na kukuta
fedha zilizotolewa na halmashauri ya wilaya hiyo sh. milioni 35 hazijafanya
kazi za kumridhisha, jambo lililofanya kuwaweka kitimoto baadhi ya wakuu wa
idara kwenye kituo hicho.
Alisema, kazi kubwa ya majengo mawili yaliyojengwa kwenye kituo hicho
ikiwemo jengo la wagonjwa wa nje (OPD), ofisi za madaktari na wauguzi
zimefanywa na wananchi huku Shirika la World Vision likitoa vifaa ikiwemo
saruji.
Mkuu wa Wilaya ya Kilindi,
Suleiman Liwowa alipigilia msumari wa mwisho baada ya kusema hata wao kama
wilaya wameona kuna 'uchakachuaji' wa fedha hizo na suala hilo wamelifikisha
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU
No comments:
Post a Comment