15 August 2013

VIONGOZI WA DINI WAONYWA KUTOJIHUSISHA NA SIASA



MKUUwaWilayayaI gunga mkoani T abo ra, Eliba rik iKinguamewaasavio ngoziw adini kutojihusish a namasual aya siasanabadala yake wajengemi singiya kirohokwawaumini ilinchi iendeleek uwanaamani,anaripoti Abdalla hAmi ri, Igunga
.Ha yoaliyasemamw ish onimwawikika tika tamas halauzin duzi waalbam u yan yimbozai njili ya, AnnaNzog iijulikan ayo kwajinalaNjo onitumwimbi e b wana uliof an yikakati ka ukumbiwaShuleyaMsingi St.Leo the Great uliopo mj ini Igunga.
A lisem a kuwabaad hiyaviongozi wadiniwameku wawa ki jihusishana masuala yasias anakuacha kumtumikiaMu nguh ali ambayoina letamfarakano katika shughuli zamae ndeleo.
Aliongezakuwabaadhiyawananchi wam ekuwa wakitum ia fedha nyingi kwakufanyamamboyasiyompendeza Mungu badala ya kuwekeza katika shughuli mbalimbali za maendeleo na kutoa sadaka.
“Ndugu waumini mliokusanyika katika tamasha hili, leo nimeona niyaseme haya kwani kuna baadhi ya watu wamekuwa wakitumia muda wao mwingi kwenda kwa waganga wa kienyeji na kudanganywa na hatimaye kujiingiza katika vitendo viovu ambavyo vinamchukiza mwenyezi mungu,” alisema Kingu.
Katika tamasha hilo lilienda sambamba na harambee ya kuchangia kwaya ya Jerusalemu ya Kanisa la Moravian mjini Igunga kwa ajili ya kusaidia watoto yatima, wajane na watoto wanaoishi katika mazingira magumu.
Aidha, katika harambee hiyo jumla ya sh.milioni 1.4 zilichangwa ambapo mkuu huyo wa wilaya alichangia kiasi cha sh.650,000.
Naye mlezi wa Kwaya ya Jerusalemu ya Kanisa la Moravian mjini Igunga, Nyanza Sulwa aliwaomba viongozi wa dini kuendelea kuliombea taifa liendelee kuwa na amani.
Alisema kuwa ili nchi izidi kuwa na amani ni vyema wananchi waendelee kumuomba Mungu kwani kumekuwa na viashilia mbalimbali vya uvunjifu wa amani ambapo watu wamekuwa wakimwagiwa tindikali na kupigwa risasi pasipo makosa yoyote.
Kwa upande wake, Mchungaji wa Kanisa la Moravian mjini Igunga, Isaya Misayo aliwataka waimbaji wa nyimbo za injili kutotanguliza masilahi mbele na badala yake wafanye kwa ajili ya kumtumikia Mungu.
Aliongeza kuwa kumekuwa na baadhi ya watu wanaotumia mambo ya dini kwa nia ya kujipatia vipato vyao binafsi na kuwaasa waachane na tabia hizo.

No comments:

Post a Comment