19 August 2013

UTOAJI HUDUMA BORA WATAJWA KUWA SIRI YA MAFANIKIO



Na Mwandishi Wetu
UTOAJ I h u d uma b o r a umetajwa kuwa ndiyo kipaumbele cha kwanza kwa wateja wa benki ya Exim na kwamba tayari imeanzisha mfumo wa kupunguza foleni katika matawi yake ikiwa ni moja ya mikakati ya kuboresha huduma kwa wakati.

Hayo yalisemwa na meneja wa huduma kwa wateja wa benki hiyo, Frank Matoro, wakati wa maadhimisho ya miaka 16 tangu ianze kutoa huduma hapa nchini.Alisema utoaji wa huduma bora ni kipaumbele kikubwa kwa benki yake na kwamba tayari benki imeshaanzisha mfumo wa kupunguza foleni katika matawi yake.
“Pia tumeanzisha huduma za kisasa ya kuwasiliana na wateja kupitia mtandao ambayo inajulikana kama Online Chat Service, kwa ajili ya wateja wetu kuwasiliana na wawakilishi wa benki kupitia mtandao watakaosaidia kutatua matatizo yao mbalimbali kwa wakati,” alisema Matoro.
Akizungumza wakati wa sherehe ya maadhimisho hayo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, ofisa mtendaji mkuu wa benki hiyo, Dinesh Arora, alisema benki yake imejikita katika utoaji wa huduma za kibenki za kipekee ikiwa na lengo la kuziba pengo la wasiofikiwa na huduma hiyo nchi nzima.
Alisema maadhimisho ya miaka 16 yamekuja yakiambatana na mafanikio ya benki hiyo kwenye sekta ya kibenki Afrika kutokana na kuorodheshwa kwenye tuzo za Benki Bora Afrika, zilizofanyika jijini Marrakesh, Morocco.
“Tutaendelea na jitihada zetu za kutoa huduma baada ya kumaliza miaka 16 yenye mafanikio makubwa,” alisema na kuongeza;“Mafanikio yetu katika kipindi hiki yametokana na dhamira yetu ya kutoa huduma za kibenki za kipekee zitokanazo na wafanyakazi, makini na wateja wetu waaminifu.”

No comments:

Post a Comment