Stella Aron
TANZANIA
ni miongoni mwa nchi duniani inayosifiwa kuwa na amani ya kudumu tangu kupata
uhuru.
Ni miongoni mwa mataifa yasiyo na
historia ya vita duniani na kupata uhuru wake bila kumwaga damu.
Aidha, mataifa ya kigeni yanapenda kuja
kuwekeza miradi na makazi huku wanaosikia habari zake wakitamani kufika kuiona
amani inayosikika kote ulimwenguni
.
Ni dhahiri kwamba Tanzania
imebarikiwa kuwa na hali ya hewa nzuri, mbuga za wanyama, rasilimali za
kutosha, maliasili ardhi na madini, misitu, milima na mabonde ambayo pekee
yanaifanya kuonekana katika mitazamo tofauti tofauti na hivyo kuwafanya watu
wengi kuja kutalii na kufanya makazi au uwekezaji.
Kwa tafakari ya kawaida hapa utagundua
amani tunayoisema ni ile ya kutokuwa na vita, mizozo, malumbano, migogoro
miongoni mwao.
Aidha, katika nchi yenye vita huwezi
kufanya kitu chochote badala yake watu wa taifa husika watakuwa ni wakimbizi na
wageni wataogopa kuja kuwekeza katika nchi hiyo.
Mwanzoni mwa miaka ya 1945 baada ya
vita vya pili ya dunia, Afrika kuliibuka vuguvugu la kudai uhuru miongoni mwa
nchi watawaliwa.
Wakati huo nchi nyingi za Afrika
zilikuwa zinatawaliwa na mataifa ya nchi za Magharibi kama
Ujerumani, Uingereza, Ufaransa, Ureno na Ugiriki.
Aidha katika kudai uhuru wake nchi hizo
zilitumia njia tatu, ambazo moja ni njia ya kudai uhuru kwa kumwaga damu au
njia ya mtutu wa bunduki, pili kudai uhuru kwa njia ya kufanya mapinduzi na
tatu njia ya amani.
Historia inaonesha kwamba katika
kujipatia uhuru wake nchi nyingi za Afrika zilipata uhuru kwa njia ya vita na
umwagaji damu.
Njia hii pekee inazijengea sifa mbaya
ya kuwa nchi za vurugu na zisizotaka makubaliano katika kufanya mambo na
mipango yake.
Tanzania
ilitumia njia ya amani ambayo pekee inaijengea sifa kubwa miongoni mwa mataifa
ya Afrika na duniani kwa ujumla.
Na hii itakumbukwa kwamba hata mara
baada ya kupata uhuru bado Tanzania
iliendelea kuwaheshimu nchi watawala bila kulipiza kisasi kama
ilivyokuwa kwa wengine.
Katika historia ya amani iliyopo usipo
mkumbuka baba wa taifa, mwalimu Julius Nyerere kwa jitihada zake katika
kulipigania taifa kupata uhuru wake pasipo vita pia, kuliongoza taifa kwa amani
ya kudumu.
Katika uhai wake Mwalimu alipigania sana suala la amani
ambalo kwa kiasi kikubwa linapigiwa kelele na mataifa mengi duniani na mwasisi
wa usuluhishi wa migogoro katika nchi za Afrika na mataifa mengine duniani.
Kama utakuwa unashuhudia kinachoendelea
katika nchi kama Somalia, Tunisia, Syria,
Misri na Libya
utakumbuka kilio cha baba wa taifa, hayati mwalimu Julius Nyerere kuhusu amani
barani Afrika.
Katika matazamo huu wa kuingalia Tanzania kama
nchi ya amani watu wanatumia vigezo vya utulivu na upendo nchini.
Katika utamaduni wa watu ambao
sitausahau ni amani ya Watanzania, tena wale wanaoishi katika maisha ya kawaida
na wageni wanaingia kila iitwapo kesho.
Lakini kama tutaendelea kusifia amani
hii pasipo kurejea misingi ya haki na usawa miongoni mwa Watanzania itakuwa ni
sawa na kazi bure.
Amani ni usalama katika haki na usawa
miongoni mwa jamii na hudhihirika katika utekelezaji na utoshelevu wa mipango
bila kubughudhi utulivu wa watu wengine.
Katika maana hii utaweza kujiuliza
maswali, je mauaji ya albino nchini ndiyo amani tunayojivunia? ukatili dhidi ya
watoto yatima na walemavu ndiyo amani tunayoisema? ukatili juu ya wafanyakazi
katika sekta mbalimbali ndiyo misingi ya Tanzania? kutokuhoji mambo na
kuonesha hisia ndiyo chanzo cha amani tunayosifiwa na mataifa mengine?
Kutokana na kwamba miongoni mwa
Watanzania bado kuna watu wanaendelea kuangamia kutokana na vurugu na matukio
yanayoendelea utakuwa ni shahidi kwa tukio lilompata Dkt. Steven Ulimboka baada
ya kutekwa na watu wasiojulikana, kwa maelezo yake akiwa katika hali mbaya ya
kujeruhiwa na watu hao anadhihirisha jinsi alivyofanyiwa unyama.
Mbali ya kusulubiwa kwa Dkt. Ulimboka
pia Mhariri wa gazeti la Mtanzania Absalom Kibanda naye alifanyiwa ukatili na
watu wasiofahamika , matukio ambayo hadi sasa yamekuwa historia kutokana na
wahusika kufanyiwa ukatili wa kutisha.
Mambo kama
haya tumezoea kuyasikia kwenye nchi za kidikteta na kuongozwa kimila ambapo
watawala badala ya kutumia njia ya kidemokrasia na kisheria kushughulikia
wanaoamini ni maadui zao katika utawala, hutumia genge la wahuni katika taasisi
za usalama kuteka raia, kuwatesa, kuwafunga na hata kuwaua.
Sitaki kuamini kwamba Tanzania
imefikia huko ukatili huo pekee unaashiria watu wenye mioyo migumu kiasi cha
kushindwa kuwa na utu na uvumilivu na kuwepo kwa ukoloni mambo leo.
Pia katika suala la maandamano
yanayofanywa nchini na vikundi mbalimbali vya wanaharakati vinaashiria moja kwa
moja kukosekana kwa amani ambayo bado tunaendelea kujivunia pasipo kuangalia
haki na usawa kama vinatiliwa mkazo.
Tanzania
ni jambo la kawaida kufanya utekelezaji wa sera na mipango mpaka pale watu
wanapoandamana, kitendo hiki kinachochea hali ya kukosekana kwa amani miongoni
mwa wananchi hata kama kuna watu wanatusifia.
Aidha, kitendo cha askari kutumia
mabomu kuwatuliza na kuwatawanya watu wakati wa kufanya maandamano kudai haki
zao za msingi kinaashiria kukosekana kwa amani miongoni mwa wazawa na inabaki
katika historia na nadharia na badala yake hatuwezi kufikia kilele cha amani ya
kudumu.
Kama utaratibu huu utaendelea kutumiwa
na watawala kama njia pekee ya kutatua
matatizo na itakuwa ni njia ya kuwapa kiburi Watanzania kiasi kwamba baadaye
nchi inaweza kuingia katika machafuko yasiyovumilika kiasi kwamba jeshi
linalotumika kutuliza amani litashindwa kufanyakazi na ndiyo mwanzo wa vita
miongoni mwetu.
Kadhalika utakumbuka utofauti uliopo
kati ya walionacho na wasionacho (maskini na tajiri). Katika nchi ya Tanzania
utabaini kuwa kuna utofauti mkubwa hali inayobainisha moja kwa moja kukosekana
kwa usawa miongoni mwa wananchi.
Kitendo hiki kinawanyima amani watu wa
hali ya chini kwani hawawezi kuyafurahia maisha yao.
Hata hivyo utofauti unafanywa na
viongozi wa ngazi za juu katika serikali unawapa hasira wananchi kutokana na
kwamba hakuna hatua zozote za kisheria zinazochukuliwa dhidi ya vitendo hivyo.
Katika mtazamo wa kawaida wapo
Watanzania wanaojilimbikizia mali
huku wakiendelea kuwakandamiza wengine na ambao kwa bahati mbaya ndiyo wavuja
jasho, asilimia kubwa ya wakulima wanafanya kazi usiku na mchana lakini bado
hali zao ziko matatani na wakati mwingine wanakosa hata mlo mmoja kwa siku.
Hebu tujiulize amani tunayojivunia ni
hii ya kutofautiana kimaendeleo miongoni mwetu kiasi kwamba hatukuzaliwa na
kukulia katika nchi moja ambayo kila siku inasemwa maskini.
Je, umaskini tunaousema ni ule wa
kukosa kunufaika na maliasili zetu na badala yake kuwanufaisha wachache?
Kama jibu ni ndiyo kwa nini tuendelee
kulea mifumo inayowanufaisha wachache na badala yake wengi kukosa amani ya kuwa
wazawa katika nchi yao?
Kama
utataka kusoma hali ya hewa ya taifa letu kumbuka mara baada ya kukamatwa mwizi
wa kuku, jinsi anavyoshughulikiwa, wakati mwingine kumchoma moto.
K a d h a l i k a k ama ama n i tunayojivunia
itakuwa ni ile ya utulivu, kukosekana kwa vita, upendo, makubaliano hatuna budi
kurudia utamaduni wetu wa usawa na haki miongoni mwetu pasipo ubaguzi wa rangi,
hali za kimaisha na kikanda.Kwani umaskini ndiyo utachangia kuvuruga amani
iliyopo
No comments:
Post a Comment