16 August 2013

PIKIPIKI NI JANGA JIPYA KWA VIJANA



ONGEZEKO la usafiri wa pikipiki nchini kwa asilimia kubwa, umeondoa usumbufu kwa wasafiri wenye kipato cha chini wasio na uwezo wa kukodi taksi.Kutokana na msongamano wa magari nchini hususan katika jiji la Dar es Salaam watu wengi hivi sasa hupenda kutumia usafiri huo ili kukwepa foleni na kuwahi wanapokwenda.

Usafiri huo umesaidia kurahisisha mawasiliano katika sehemu ambazo barabara hazipitiki kirahisi.Wakati hayo yanajiri magari madogo ya abiria yameathirika kutokana na kuwepo usafiri huo kwani pamoja ni usafiri wa haraka sana na bado siyo ghali kwa wasafiri ukilinganisha na bei za magari madogo kwa safari moja.
Vyombo hivyo vilianza kutumika baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitisha sheria ya pikipiki na bajaji kutumika kubeba abiria.Pikipiki hizo zimekuwa ni sehemu ya ajira kwa vijana wengi, kujipatia namna zao za kuishi na kuendesha familia zao.
Pamoja na faida hizo, pia kuna hasara nyingi zilizoletwa na usafiri huo, ikiwa ni pamoja na ajali nyingi zinazotokana na pikipiki hizo na majeruhi.Pamoja na kuwepo kwa usafiri huo lakini tayari umesababisha ajali nyingi ikilinganishwa na magari na kupoteza maisha ya raia wasio na hatia na wengine kupata vilema vya kudumu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uzembe wa madereva hao.
Ajali na majeruhi vimefanya vijana waliokuwa wakitegemewa na familia zao, kugeuka kuwa tegemezi badala ya kutegemewa, idadi kubwa ya Watanzania wamepata vilema vya kudumu.
Madereva wengi nchini hawana leseni wala mafunzo ya uendeshaji pikipiki kwa mujibu wa sheria ambao wengi walijiingiza huko kutokana na kukosa ajira.
Uchunguzi uliofanywa unaonesha kuwa, idadi kubwa ya vijana hao hawana mafunzo ya udereva na usalama barabarani. Ndiyo maana wengi wao wanaendesha bila kufuata kanuni na sheria.
Pamoja na usemi wa ajali haina kinga, bado ajali nyingi zinazotokea kwa uzembe zinazosababishwa na uharaka na kuacha kufuata sheria za barabara zinavyosema na kuelekeza.
Tanzania kwa sasa ipo katika hatari ya kupoteza nguvu kazi kutokana na ongezeko kubwa la ajali na kusababisha hali ngumu ya maisha kwa wanaowategemea.
Ongezeko la magari na pikipiki nchini limekuwa tatizo kama siku za nyuma simba walivyokuwa wanajeruhi, kula watu na kuhatarisha maisha ya wananchi.
Mwaka 2008 kulikuwa na ajali za barabarani 17,451 na kusababisha vifo 2,460 na majeruhi 16,982.
Mwaka 2009 kulikuwa na ajali 22,019 na kupoteza uhai wa watu 2,872, waliokufa 3,851 na waliojeruhiwa walikuwa 20,717.
Tofauti yake ilikuwa 4,568 sawa na asilimia 26.2.
Ajali zilizosababisha vifo ilikuwa 412 sawa na asilimia 16.7, waliokufa 1,011 sawa na asilimia 35.6 na waliojeruhiwa 3,735 ambapo ni asilimia 22.
Mikoa iliyoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya ajali za barabarani ilikuwa Dar es Salaam 6,538 na mwaka 2009 ilikuwa 9,312, Pwani ilikuwa ya pili kwa ajali 1,315 lakini mwaka 2010 matukio ya ajali 1,239 na kufanya Mkoa wa Arusha kuwa wa pili kwa idadi ya ajali 1,681.
Takwimu zinaonesha kuwa, kadiri miaka inavyoenda ajali zinazidi kuongezeka pia badala ya kupungua huku matumaini ya kumaliza tatizo hilo yakipotea.Mwaka 2010 zilitokea ajali 24,926 na kusababisha vifo 3,687, majeruhi 22,064 ambapo ajali nyingi zilisababishwa na pikipiki.
Kutokana na takwimu hizo, 2009, vyombo vya moto vilivyosajiliwa vilikuwa 624,909, pikipiki zilikuwa 207,465 sawa na asilimia 33.1.
Ajali za pikipiki pekee mwaka 2009 zilikuwa 3,945 na kupoteza nguvu kazi ya watu 385 na majeruhi 2,666.
Kutokana na usafiri wa pikipiki kuwa mbadala kwa wananchi wengi tayari imesababisha ongezeko la mahitaji yake kwa matumizi ya kila siku.
C h a n g a m o t o k u b w a k w a waendesha pikipiki ni wizi ambapo mwaka 2009 ziliibwa 859 na 2010 idadi hiyo iliongezeka na kufikia 1,615 kutokana na ongezeko la pikipiki kwa asilimia 87.9.
Kutokana matukio haya kikosi cha usalama barabarani kinatakiwa kuangalia upya namna ya kudhibiti ongezeko la ajali zinazosababishwa na pikipiki.
Kwanza waangalie leseni zao ili kuwabaini wasiokuwa nazo, pia sheria za barabarani zifuatwe na wanaokiuka wachukuliwe hatua kali kinyume na hivyo tutazalisha kundi la watu vilema.
Elimu usalama barabarani inatakiwa kutiliwa mkazo ili kupunguza ajali hizo, pia leseni zitolewe kihalali baada ya kupata mafunzo kama madereva wengine.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga kwa kushirikiana na watendaji wake bado wana kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa vijana wengi wanaoendesha pikipiki wanapata elimu ya usalama barabarani pamoja na kupata mafunzo ya uendeshaji pikipiki.
Hivi sasa katika maeneo mengi ya jiji vijana wengi wamejiajiri bila ya kuwa na elimu yoyote ya usalama barabarani na pasipokuwa na leseni jambo ambalo limekuwa likichangia kuongezeka kwa ajali na kuonekana sasa suala la ajali za pikipiki ni ugonjwa.
Asilimia kubwa ajali zinazotokea kila siku nyingi huwa zinatokana na pikipiki hivyo kuna haja sasa ya kuboresha utoaji wa elimu ya usalama barabarani na kuhakikisha kuwa vijana wanapata mafunzo ya udereva ikiwa ni pamoja na kuwafuata kwenye vituo vyao ili kuinusuru nguvukazi ya taifa la

No comments:

Post a Comment