30 August 2013

TPAWU YAPINGA KIMA CHA MSHAHARA



 Na Rehema Maigala
MW E N Y E K I T I wa Kama t i y a W a n a w a k e mashambani na Kilimo (TPAWU), Patricia K i s h i m b a a m e s e m a hawakuridhishwa na kima cha chini cha mshahara kilichotangazwa na Serikali sh 100,000
. Akizungumza katika kikao cha utendaji cha wanawake alisema walijadili kuhusu kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa mashambani na kuona haufai kulingana na maisha yalivyo sasa. "Hatukuridhishwa na kima hicho cha mshahara kulingana na maisha ya sasa yalivyo hivyo hivi sasa tumeaandaa mapendekezo kwa ajili ya kuyapeleka serikalini kwa ajili ya kutuongezea kiasi hicho cha pesa," alisema Kishimba.
Aliongeza kuwa Serikali inatakiwa kuangalia upya kima hicho cha mshahara ili nasi tuweze kufanya kazi kwa bidii na kwa tija zaidi. Naye Mwenyekiti wa Taifa wa (TPAWU), Jaicy Kayera alisema watafanya mkutano mkuu wa chama hicho ambapo kwa hivi sasa itakuwa ni mara ya kwanza kwa chama hicho kufanya mkutano huo.
Alisema lengo la kikao hicho ni kuangalia kazi za chama tangu miaka saba iliyopita kuangalia mapitio ya katiba ya chama kwani wa n a c h ama wa l i t a k a katiba ya sasa iboreshwe na kuangalia hali halisi ya wafanyakazi na sheria za kazi zilizopo. Hata hivyo, Kayera alisema chama chao kina mikutano mikuu miwili ambayo ni mkutano mkuu na mkutano wa kazi

No comments:

Post a Comment