Na Abdallah Amiri, Igunga
JESHI la
Polisi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora jana lilimfikisha mahakamani, Msua
Malanda (37), mkazi wa kijiji cha Segerei, Kata ya Igoweko wilayani Igunga kwa
kosa la kumpiga mumewe chupa kichwani na kusababisha kifo chake.
Akisomewa shtaka mbele ya
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Igunga, Ajali Milanzi, Mwendesha
Mashtaka wa Polisi, Dezidery Kaigwa, aliiambia mahakama kuwa mshtakiwa
anakabiliwa na kosa la kusababishia kifo.
Mwendesha mashtaka huyo alidai
kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 196 (A) kanuni ya
adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 ambapo inazuia kufanya
makosa kama hayo.
Aliiambia mahakama kuwa Agosti
24, mwaka huu saa 5:00 asubuhi katika Kijiji cha Segerei kata ya Igoweko
wilayani hapa mshtakiwa alimpiga chupa kichwani mume wake, Abdallah Hamisi (48)
na kumsababishia kifo.
Baada ya kusomewa shtaka hilo
mshtakiwa hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza
kesi hiyo.Mshtakiwa alirudishwa rumande na kesi hiyo
imeahirishwa hadi Septemba 13, mwaka huu, itakapotajwa tena
No comments:
Post a Comment