29 August 2013

TBS WARUHUSU MAFUTA YA OKI



Na Grace Ndossa
SHIRIKA la Viwango nchini (TBS) limesema mafuta ya kula aina ya OKi yanaruhusiwa kusambazwa kwenye soko la ndani baada ya kubainika hayana madhara. Uamuzi huo unatolewa zikiwa zimepita siku kadhaa, TBS kutangaza kwa umma kuwa mafuta hayo ambayo yanazalishwa nchini Malaysia hayafai kwa matumizi ya binadamu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo jana, Joseph Masikitiko ilieleza kuwa uchunguzi waliofanya kwa kushirikiana na Tume ya Ushindani (FCC) waligundua kuwa mafuta hayo hayana matatizo kiafya.
Taarifa hiyo, ilieleza kuwa baada ya uchunguzi wa kina kuonesha hayana madhara wamemtaka mzalishaji wa mafuta ya OKi kuteua wakala ambaye atahusika na uingizaji na usambazaji wa mafuta hayo nchini. Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa, mzalishaji anatakiwa kuuza kwa wakala mafuta ya ujazo wa lita 10-20 tu katika vifungashio vya madumu ya plastiki.
"Mafuta ya Oki yanaruhusiwa kusambazwa na kuuzwa kwenye soko la Tanzania baada ya uchunguzi yakinifu uliofanywa na shirika kwa kushirikiana na Tume ya Ushindani (FCC), mzalishaji wa mafuta hayo na kubaini tatizo ni mafuta bandia yanayoingizwa nchini kupitia njia za panya na kuuzwa na wafanyabiashara wasio waaminifu," alisema Masikitiko.
A l i s e m a , T B S k w a kushirikiana na Tume ya Ushindani watahakikisha mafuta ya OKi yanaingia nchini kwa utaratibu uliokubalika na yatapewa alama ya ubora. Pia alisema, mafuta ya Oki ya ujazo wa lita moja hadi tano ambayo yamepimwa na kukutwa hayakidhi viwango hayaruhusiwi kuuzwa na ruhusa hiyo haitahusu mafuta ya kupikia ya Viking na ASMA, kwa kuwa mpaka sasa wazalishaji na wafanyabiashara wa mafuta hayo hawajapatikana wala kujitokeza ili kushughulikia matatizo yanayohusu bidhaa zao.

No comments:

Post a Comment