Na Anneth
Kagenda
KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali
(PAC), Serikali za Mitaa na Kamati ya Bajeti, zimeitaka Serikali itumie mashine
za kieletroniki kutokana na ukosefu wa taarifa sahihi kuhusu deni la Taifa
ambapo upo umuhimu mkubwa wa kukutanisha wadau kama Benki Kuu (BoT) na
hazina.Mwenyekiti wa PAC, Bw. Zitto Kabwe, aliyasema hayo jana katika taarifa
yake kwa vyombo vya habari na kuongeza kuwa, hayo ni kati ya maazimio
yaliyopitishwa na kamati hizo.
Al i s ema k ama t i h i z o
zimeishauri Serikali kuunda c h omb o h u r u amb a c h o kitasimamia deni la
Taifa ambapo Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, haiweki uwazi wa kutangaza
umiliki wa mali za viongozi.Bw. Kabwe aliongeza kuwa, hali hiyo
inasababisha viongozi kutoweka wazi mali wanazomiliki hivyo ni rahisi mtu
kuzushiwa umiliki wa mali usio wa ukweli.
"Ni vyema Sekretarieti ikafanya
utafiti juu ya umiliki wa mali kwa viongozi wa Umma na kuweka taarifa hizo
katika tovuti ya Sekretariati ili kuwawezesha wananchi kuona mali
zinazomilikiwa na viongozi wao.
Aliongeza kuwa, kwa kuwa hivi sasa
leseni za udereva zinaweza kuweka kumbukumbu za makosa ya usalama barabarani,
Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), ikishirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi, kuhakikisha askari wa Usalama Barabarani wanatumia utaratibu huo wa
kisasa wa kutoza faini na kutoa risiti za malipo za elektroniki.
Alisema kamati zimeridhia maduhuli ya
Serikali, yakusanywe kwa kutumia risiti za elektroniki ambapo Serikali Kuu,
Serikali za Mitaa na Mashirika ya Umma, yaanze kutumia risiti za eletroniki
mara moja kudhibiti upotevu mapato ya serikali.
"Pia tumekubaliana ofisi zote za
Serikali zifanye manunuzi yake kwa wafanyabiashara wanaotumia mashine za
kielektroniki pamoja na kufanyiwa mabadiliko kwa sheria ya "The Proceeds
of Crime Act, 1991".
"Sheria hii tunataka iwekwe kifungu
kinachomwezesha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mkurugenzi wa Mashtaka
nchini (DPP", kuwa na mamlaka ya kuomba mahakama kufungua kesi ya madai
kwa watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi," alisema
No comments:
Post a Comment