Na Ester Maongezi
WANYANGE 15 kutoka katika vitongoji
vinne vya Wilaya ya Ilala, wameanza mazoezi ya kumsaka mrembo wa Redd's Miss
Ilala 2013 yanayofanyika katika Ukumbi wa klabu Billicanas uliopo katikati ya
Jiji la Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa
mratibu wa mashindano hayo, Juma Mabakila, alisema mashindano hayo yanatarajia
kufanyika Agosti 16, mwaka huu katika Ukumbi wa Golden Jubilee Tower, ambapo
warembo watatu watakaoshika nafasi za juu watashiriki Redd's Miss Tanzania
2013.
Mabakila
alisema warembo hao wanatoka katika vitongoji vya Mzizima, Tabata, Ukonga na
Dar City Centre.Al i s ema ma a
n d a l i z i y a mashindano hayo, yanaendelea vizuri na wamepania kuonesha
vipaji vyao katika mchuano utakaofanyika wiki ijayo.
"Sisi kama kamati tunawaomba wadau
wa urembo kujitokeza kwa wingi kuja kushuhudia muonekano mpya wa mashindano ya
urembo, lakini pia kuangalia jinsi Ilala ilivyosheheni warembo watakaoleta
ushindani mkubwa Redd's Miss Tanzania 2013," alisema.
Aliwataja warembo waliopo katika kambi
ya Miss Ilala ni Alice Isaac, Clara Poul, Anna Johnson, Iren Mwelolo, Munira
Mabrouk, Rehema Mpanda, Shamim Mohamed, Martha Gewe, Diana Joackim, Natasha
Mohamed, Dorice Mollel, Pendo Lema, Kazumbe Mussa na Kabula Kibogoti.Alisema hadi sasa kampuni zilizojitokeza kuwadhamini ni
Redd's, Dodoma Wine, CXC Tours, Chilly Will, Clouds FM, City Lounge, Times FM
na Lemutuz Blog.
No comments:
Post a Comment