15 August 2013

RAIS KUWAADHIBU MAWAZIRI WAZEMBE



Na Amina Athumani
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wassira amesema Rais Jakaya Kikwete amesisitiza atawajibisha mawaziri wote watakaozembea kutimiza majukumu yao ikiwemo mipango ya maendeleo nchini.

Hayo aliyasema juzi jijini Dar es Salaam wakati akieleza mkakati wa Serikali katika kutekeleza mfumo ujulikanao kama 'Matokeo Makubwa Sasa'. Waziri Wassira alisema, katika utekelezaji wa mfumo huo watendaji hasa mawaziri watakaozembea majukumu yao watawajibishwa na kiongozi mkuu wa Serikali ambaye ni Rais.
Alisema, lengo la mfumo huo ni kuleta matokeo mazuri ya uchumi kwa muda mfupi. Pia alisema, mfumo huo utagharimu zaidi ya sh. trilioni 8.9 kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano, ambapo Serikali itawekeza kiasi cha sh. trilioni 2.9 huku sekta binafsi zikitarajiwa kuwekeza sh. trilioni 6.
Alisisitiza kuwa, mafanikio ya mfumo huo yatategemea na ushiriki mkubwa kutoka katika sekta binafsi
Wa z i r i Wa s s i r a alizihakikishia sekta binafsi kwamba Serikali iko pamoja nao katika shughuli za kibiashara.
Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watendaji Wakuu wa Taasisi na Makampuni Binafsi nchini, Ally Mafuruki alipongeza hatua ya Serikali kusitisha kuagiza samani nje ya nchi kwa ajili ya matumizi ya Serikali ambayo sasa itazinunua katika soko la ndani. Mwenyekiti huyo pia ameitaka Serikali iweke v i g e z o v y a u b o r a i l i wazalishaji wa ndani wa samani hizo wazitimize.

No comments:

Post a Comment