30 August 2013

RAGE AIRUDISHA SIMBA DAR KUCHEZA NA MAFUNZO



 Na Elizabeth Mayemba
MWENYEKITI wa klabu ya Simba Aden Rage ameamuru timu hiyo irudi Dar es Salaam kwa ajili ya kucheza mechi ya kirafiki na Mafunzo ya Zanzibar itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa lengo la kuwatambulisha wachezaji wao kutoka Burundi
.Wachezaji hao ni Amisi Tambwe, Gilbert Kaze na kiungo wao za zamani Henry Joseph aliyetokea katika klabu ya Kongsvinger ya Norway.Beki Kaze na mshambuliaji Tambwe awali walishindwa kutambulishwa baada ya kushindwa kupatia Hati zao za Uhamisho (ITC), ambapo kwa sasa tayari wamepatiwa.
Awali Kocha Mkuu wa timu hiyo Abdallah Kibadeni alikataa timu kucheza mechi hiyo kwa madai icheze Moshi mkoani Kilimanjaro baada ya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania na JKT Oljoro, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha, ambao Simba ilishinda 1-0.
Hata hivyo baada ya viongozi wa juu kukaa wakakubaliana timu yao icheze na Mafunzo ya Zanzibar badala ya Machava FC ya Moshi.Rage alilazimika kwenda Burundi kufuata ITC za wachezaji hao mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kuona zinachelewa kufika nchini, hivyo kuwachelewesha pia kuanza kazi.
Wachezaji wengine wa kigeni wa Simba, Waganda Joseph Owino na Abel Dhaira, wamecheza mechi zote mbili za awali za Ligi Kuu, kutokana na kukamilishiwa taratibu zote za uhamisho na kuwa na vibali vya kufanya kazi nchini.
K a z e n a T a m b w e waliosajiliwa kutoka mabingwa wapya wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati,Kombe la Kagame, Vital'O ya wakati wa ufunguzi wa Ligi Kuu walikuwapo Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi, Tabora kuishuhudia timu yao ikilazimishwa sare ya 2-2 na Rhino Rangers.

No comments:

Post a Comment