30 August 2013

CHEKA,WILLIAMS KUDUNDANA LEO



 Na Fatuma Rashid
MABONDIA Phil Wiliums wa Marekani na Francis Cheka, wamepima uzito kwa ajili ya pambano lao la ngumi la ubingwa wa WBF la uzito wa kati linalotarajiwa kufanyika leo, kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa kupima uzito huo, Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO) ambao ni wasimamizi wa ndani wa mpambano huo, Yassin Abdallah 'Ustaadhi' alisema pambano hilo litautafanya mchezo wa ngumi kuzidi kusonga mbele nchini.
Ustaadhi alisema katika sheria za Shirikisho la Kimataifa la Ngumi za Kulipwa (WBF), bondia anatakiwa kutetea mkanda huo ndani ya miezi tisa."Bondia atakayenyakua mkanda huu atatakiwa kuutetea kwa muda wa miezi tisa na hatoruhusiwa kushiriki mpambano wowote hadi pale atakapoomba na kuruhusiwa na WBF," alisema.
Alisema pambano lingine kati ya Alphonce Mchumiatumbo na Deandre Mccole kutoka Marekani katika uzito wa juu usio wa ubingwa, halitachezwa kutokana na bondia huyo wa Marekani kuchelewa kuwasili nchini.

No comments:

Post a Comment