Na Kassim Mahege
MKAZI
wa Kijiji cha Kanga wilayani Chunya mkoani Mbeya, Maria Martin (37),ameuawa kwa
kupigwa ngumi kichwani na kukabwa shingoni na mpenzi wake kutokana na wivu wa
kimapenzi. Kwa mu j i b u wa t a a r i f a iliyotumwa kwa vyombo vya habari na
Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Diwani Athumani ilisema mkazi huyo alipatwa na
mauti hayo Agosti 13, mwaka huu saa 6.05 usiku. “Mtuhumiwa alifahamika kwa jina la Lameck Msangawale (35) ambaye alikimbia mara baada ya tukio
kutokea,”ilisema taarifa hiyo.
Taarifa ilifafanua zaidi kuwa chanzo cha mauaji
hayo ni kutokana na wivu wa kimapenzi baada ya mtuhumiwa kumkuta marehemu akiwa
na mwanaume mwingine. Aidha Kamanda Athumani ametoa rai kwa mtu yeyote mwenye
taarifa juu ya mahali alipo mtuhumiwa kutoa taarifa katika mamlaka husika ili
sheria ifuate mkondo wake. Katika hatua nyingine, mkazi wa Mbozi mkoani Mbeya,
Sijaona Haonga mwenye umri wa miaka 45 ameuawa kwa kunyongwa shingoni kisha
kutupwa kwenye mto unaojulikana kwa jina la Mlowo na watu wasiojulikana.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda Athumani ilisema kuwa chanzo cha
mauaji hayo ni kutokana na mgogoro wa mashamba ambapo ulitokea kati ya marehemu
na Shabani Mbwili ikiwa ni pamoja na Mawazo Mbwili ambapo walitoroka mara baada
ya tukio. Taarifa ilifafanua zaidi alisema mbinu iliyotumika kumuua marehemu
aliviziwa wakati akivua samaki ambapo pembeni ya mwili wake kulikutwa ndoano ya
kuvuliwa samaki.
Aidha mwili wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi na daktari ikiwa ni
pamoja na kuukabidhi kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya taratibu za mazishi. Kamanda
Athumani alitoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi
badala yake kuitatua migogoro yao
kwa njia ya mazungumzo ili kuepusha
mauaji yanayoweza kuepukika.
No comments:
Post a Comment