Na Isaac
Mwangi, EANA
BARAZA la Vyuo Vikuu Afrika Mashariki
(IUCEA) limeanzisha ushirikiano na Baraza la Biashara la Afrika Mashariki
(EABC) katika juhudi mpya za kuunganisha viwanda na wasomi katika kanda hiyo.T
a a s i s i h i z o m b i l i , zinazofanyakazi kwa ushirikiano wa karibu na
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa pamoja wameandaa Kongamano na Maonesha ya
Wosomi na Sekta Binafsi 2013 yatakayofanyika baadaye mwaka huu.
Tukio hilo
linatarajiwa kufanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Kenyatta, nchini Kenya
Oktoba 23-25.
Akihutubia mkutano wa
waandishi wa habari mjini Nairobi Kenya, baada ya, maandalizi ya kongamano
hilo, Katibu Mtendaji wa IUCEA, Prof. Mayunga Nkunya alisema watu wapatao 300
wanatarajiwa kushiriki katika kongamano hilo mwaka huu.
Huku ikitarajiwa
kuvileta pamoja vyuo vikuu 102 kutoka Afrika Mashariki yote, kongamano hilo
linatarajiwa kuvutia wengi kutoka maeneo mbalimbali duniani. Taasisi binafsi
zipatazo 50 zinatarajiwa kuhudhuria kongamano hilo la siku tatu."Kongamano hili
litawaleta pamoja wasomi na sekta binafsi ili kuzalisha kile kinachotakiwa
kwenye soko,'' Prof. Nkunya alisema na kuongeza kuwa vyuo vikuu havina budi
kufundisha kile kinachohitajika na siyo kufundisha tu bila maana yoyote".
"Mgando wa mawazo
hauna budi kubadilika katika mazingira mapya ya kiuchumi tuliyonayo...vyuo
vikuu ni lazima vifanye kazi kwa pamoja na sekta binafsi,'' alisisitiza.Hili litakuwa kongamano la pili kuandaliwa na taasisi hizo mbili katika
juhudi za kuunganisha elimu ya juu na viwanda, Shirika Huru la Habari la Afrika
Mashariki limeripoti
No comments:
Post a Comment