22 August 2013

MZUNGU ANAYEDAIWA KUIBA KWENYE ATM AWEKWA KIPORO



Na Rachel Balama
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, inatarajia kutoa uamuzi wa dhamana dhidi ya raia wa Bulgaria, Todor Peev Peev (38), Mkazi wa Mbezi Beach aliyefikishwa mahakamani hapo akikabiliwa na makosa 20 ya wizi wa fedha kwenye mashine za ATM Agosti 27, mwaka huu
.Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Waliarwande Lema, alisema kuwa kutokana na mabishano baina ya upande wa serikali na mawakili wa mshtakiwa, mahakama itatoa uamuzi kama mshtakiwa atapata dhamana au la kwa mujibu wa sheria.
Mawakili wa mshtakiwa Aren Mwakyoma na Mathias Kisengu, waliiomba mahakama impatie mteja wao dhamana kwa kuwa ni raia wa Tanzania na makazi yake ni jijini Dar es Salaam na ana watoto wawili ambao wanamtegemea.
Wakili Kisengu, alisema kuwa pia mshtakiwa wakati anakamatwa aliumizwa na kushonwa nyuzi sita hivyo akiwa nje ni rahisi sana kupata matibabu.Awali, ilidaiwa kuwa Julai 28 na Agosti mosi, mbili, tatu na nne mwaka huu, maeneo mbalimbali Jijini Dar es Salaam, mshtakiwa aliiba fedha kwenye akaunti mbalimbali kwenye mashine za ATM zaidi ya sh.

No comments:

Post a Comment