13 August 2013

MWINGEREZA ANASWA NA MENO YA TEMBO



Goodluck Hongo na Revina
John
JESHI la Polisi nchini kwa kushirikiana na Idara ya Wanyamapori limemkamata r a i a w a U i n g e r e Robart Dewar (64), akiwa na nyara mbalimbali za Serikali ikiwemo meno ya tembo nane yanayokadiriwa kuwa na thamani ya sh.milioni 118.4 Raia huyo pia anadaiwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trans Africans Ligostics Limited (TALL) hapa nchini. 

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, SSP Advera Senso ilieleza kuwa mtuhumiwahuyo alikamatwa Agosti 9, 2013 saa 2:30 usiku huko Mbezi Beach akiwa na nyara hizo yakiwemo pia meno ya simba 20 na kucha 22. Taarifa hiyo ilifafanua kuwa, mtuhumiwa alikamatwa na nyara hizo zikiwa na uzito wa kilo 24 na vinyago vilivyotengenezwa kwa meno ya tembo 11 pamoja na ganda moja la bomu lenye ukubwa wa milimita 130.
Alisema, mbali na kukamatwa na nyara hizo lakini pia mtuhumiwa huyo alikamatwa na shanga mbalimbali 15 zilizotengenezwa na meno ya tembo ikiwemo pia ndege mmoja aina ya kasuku. “Tumemkamata raia wa Uingereza akiwa na nyara za Serikali, vikiwemo vipande nane vya meno ya tembo, vinyago 11 vilivyotengenezwa kwa meno ya tembo, meno 20 na kucha 22 za Simba, shanga 15 zilizotengenezwa kwa meno
ya Tembo, ndege mmoja aina ya kasuku, vipande vya miti ya mpingo.“Na idadi kubwa ya vinyago ambavyo haviruhusiwi kumilikiwa na mtu yeyote bila kibali cha Idara ya Misitu, ganda moja la bomu lenye ukubwa wa milimita 130 na mawe mbalimbali yanayodhaniwa kuwa ni madini,”alisema SSP Senso. Alibainisha kuwa, mtuhumiwa huyo alikamatwa kutokana na wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kwa kuwaambia
kuwa mtuhumiwa huyo anamiliki nyara mbalimbali za Serikali nyumbani kwake na wakati mwingine huzisafirisha sehemu mbalimbali duniani na ndipo walipomfuatilia na kumtia mbaroni.Aliongeza kuwa, mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi wake kukamilika na kuwaomba wananchi kuongeza kasi ya kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili kukomesha biashara haramu ya usafi rishaji wa nyara za Serikali. Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la watu kukamatwa na meno ya tembo ikiwemo ndani na nje ya nchi hali inayoendelea kuhatarisha kutoweka kwa wanyama hao kutokana na kuuawa kwa kasi kubwa na meno yake kusafi rishwa nje ya nch

2 comments:

  1. Anatafuta utajiri wa haraka. Wakamateni pia walio muuzia. Uroho kazi yake ni kuumia. Kaumia tayari huyo.

    ReplyDelete
  2. maskini simba na tembo wetu. naona wamnajuta kuzaliwa bongo manake nchi hii full michosho.

    ReplyDelete