Na
Ester Maongezi
CHAMA Cha
Mieleka Tanzania (AWATA), kimeandaa michuano ya Nyerere Day, inayotarajia
kufanyika Oktoba 9 mpaka 14 mwaka huu, baada ya kushindwa kufanikisha
mashindano ya Mashujaa ya mwezi uliopita.Akizungumza Dar es Salaam jana
Mwenyekiti wa AWATA, Andrew Kapelela alisema michuano ya Mashujaa ilishindwa
kufanyika kutokana na Uchaguzi Mkuu wa chama hicho.
"Tulishindwa kuandaa
michuano ya Mashujaa kutokana na kuwa katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa viongozi,"
alisema.Kapelela alisema mchakato wa uchaguzi huo ulikuwa
mkubwa kwa kuwa chama walitakiwa viongozi watakaoiendesha AWATA kwa umakini.
Aliongeza kalenda ya michuano hiyo iliingiliana na
uchaguzi huo, ambao ulikuwa unasubiriwa kwa hamu kutokana na kwamba wanachama
walihitaji mabadiliko ya kiutendaji.
Kapelela alisema michuano ya Nyerere Day itahusisha
klabu zote zilizosajiliwa Tanzania Bara na kuzitaka kujiandaa kikamilifu.Mwenyekiti huyo alisema katika
michuano hiyo ya Nyerere Day, bingwa atakabidhiwa kombe.
No comments:
Post a Comment