Anneth
Kagenda na Salma Mzee
WAFANYAKAZI wa
Mamlaka ya Reli ya Tanzania
na Zambia (TAZARA), wamesema
kama Serikali italazimisha treni hiyo iendelee
na safari zake, wasilaumiwe kwa lolote ambalo linaweza kutokea kwa abiria
wanaosafiri
.Tahadhari hiyo imetolewa Dar es Salaam
jana na wafanyakazi wa mamlaka hiyo wakati wakizungumza na gazeti hili katika
Ofisi za TAZARA na kudai mgomo wao uko pale pale hadi uongozi utakapowalipa mishahara yao
ya miezi minne
Walidai kushangazwa
na kauli za viongozi mbalimbali wanaosema mgomo huo si halali wengine
wakichanganya masilahi ya wafanyakazi hao na siasa.Walisema kitendo cha kupelekewa askari
katika ofisi hizo ili wapigwe mabomu, hakiwezi kumaliza tatizo lililopo; hivyo
wataendelea kukaa eneo hilo kwani hawapo tayari kuendelea na kazi bila kulipwa
stahiki zao.
"Tutaendelea kugoma hadi
kieleweke...tunamtaka Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda aje kusikiliza madai
yetu...kama Serikali italazimisha tusafiri kabla hatujalipwa stahiki zetu,
lolote linaweza kutokea tukiwa safarini," alisema mmoja wa wafanyakazi hao
(jina tunalihifadhi).
Alisema uongozi wa TAZARA umekuwa
ukiwatumikisha bila kujali kama wafanyakazi wanafamilia ambazo zinahitaji
huduma, kulipia pango la nyumba, ada za watoto wao na huduma nyingine za msingi
kama chakula.Bi. Theresia Mahagatile, ambaye alidai
kupewa barua ya kusimamishwa kazi na uongozi wa mamlaka hiyo, alisema kitendo
hicho ni unyanyasaji mkubwa kwani alichokuwa akikidai ni haki yake ya msingi
kama mfanyakazi.
"Kimsingi sijatendewa haki kwa
kupewa barua bila kuangalia upande wa pili...naungana na wafanyakazi wenzangu
kusema hatuondoki hapa TAZARA hadi tulipwe," alisema.Wafanyakazi hao walikusanyika na kuimba nyimbo za mshikamano ambapo
mgomo huo ulianza wiki iliyopita wakidai mishahara ya miezi minne.
No comments:
Post a Comment