15 August 2013

HALMASHAURI YAINGIA KATIKA KASHFA NZITO



Na Queen Lema, Meru
HALMASHAURI ya Meru mkoani Arusha imeingia katika kashfa baada ya kutoa zabuni kwa mkandarasi ambaye hana ofisi wala makazi maalumu kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji katika baadhi ya vijiji hali ambayo imesababisha halmashauri hiyo kushindwa utoa huduma bora ya maji kwa wananchi.

 Hayo yamebainika mara baada ya Naibu Waziri wa Maji, Binilith Mahenge baada ya kutembelea
baadhi ya miradi ambayo ipo chini ya halmashauri ambapo inadaiwa kuwa halmashauri hiyo ni moja ya
halmashauri yenye vyanzo vingi vya maji lakini haina maji.
 Akisoma taarifa hiyo Mhandisi wa Maji wilaya hiyo, Maningo Mohamed alidai kuwa kwa kipindi cha mwaka 2010 mpaka Aprili mwaka jana mkandarasi kutoka katika Kampuni ya Free World Co. Ltd aliingia mkataba na halmashauri hiyo kwa malengo ya kufanya kazi lakini hakuweza kufanya kazi hiyo na badala yake alikuwa anatoa visingizio vikiwemo vya kucheleweshewa bajeti ya Serikali kwenye sekta ya maji.        
Mhandisi Mohamed alidai kuwa mara baada ya kupewa mkataba mkandarasi huyo aliisumbua halmashauri kwa kuwa hakuwa na vifaa lakini pia hata ofi si hali ambayo iliendelea kukwamisha miradi ya maji katika wilaya hiyo hivyo kusababisha madhara makubwa ya uhaba wa maji. “Hi i k amp u n i i l i p ewa mkataba lakini kwa bahati mbaya walidanganya kuwa wana ofi si baada ya kuwafuatilia kwa undani tuliweza kujua na kutambua kuwa hana uwezo lakini tulishindwa kumuondoa kutokana na sheria juu ya wakandarasi zinavyobana,”aliongeza mhandisi huyo. 
Akiongelea uhaba wa maji katika wilaya hiyo alidai kuwa linaendelea kukua kwani kwa sasa lita zinazohitajika ni lita za ujazo elfu kumi na tano mia tano wakati zinazozalishwa ni lita elfu sita tu kwa siku jambo ambalo linasababisha uhaba mkubwa wa maji. Mhandisi Mohamed alibainisha kuwa uhaba huo wa maji unasababisha madhara makubwa kwani wananchi wa wilaya hiyo wanalazimika kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kutafuta maji huku shughuli za kila siku zikiwa zinakwama.
Awali Naibu Waziri wa Maji, Dkt. Mahenge alidai kuwa suala la mkandarasi ambaye hana ofi si wala vifaa ni la kuhuzunisha kwani huo ni uzembe wa baadhi ya watendaji wa halmashauri hiyo kushindwa kuwakagu wakandarasi kabla ya kuwapa mikataba ya kazi. Dkt. Mahenge alisema kuwa suala hilo linatakiwa kuwa la
kwanza na la mwisho na uongozi wa Halmashauri unatakiwa kuomba hata msaada kwa makandarasi wakorofi kwani wanasababisha hata miradi ya halmashauri ikiwemo maji kukwama. Aliwataka hata viongozi wa Halmashauri nao kuhakikisha kuwa wanatafuta mbinu mbalimbali za kuongeza kiwango cha uzalishaji wa maji kwani huduma ya maji iliyopo bado haiwatoshelezi kabisa wananchi ingawaje wilaya hiyo ni moja ya wilaya hapa nchini yenye vyanzo vya kutosha vya maji.

No comments:

Post a Comment