20 August 2013

MAJAMBAZI YAUWAWA DAR



 Na Leah Daudi
MAJAMBAZI wawili wameuawa na wananchi wenye hasira baada y a k ump o r a f e d h a mfanyabiashara, Wiliam Mathias mkazi wa Kijitonyama jijini Dar es Salaam.Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema tukio hilo lilitokea Agosti 18, mwaka huu, saa saba mchana maeneo ya Tazara.

Alisema, majambazi yaliyouawa yalitambulika kwa majina ya Said Hemed (42) mkazi wa Temeke Mikoroshini na Robert Aloyce (37), mkazi wa Mabibo wilayani Kinondoni ambapo siku ya tukio yalikuwa na pikipiki mbili aina ya Boxer T 665 CJR huku nyingine ikiwa imefutika namba.
"Hali hii inaonesha kuwa, wananchi wana hasira na vitendo wanavyofanyiwa na majambazi, hivyo waliamua kuwashambulia kwa mawe na kuwaua wahalifu hao," alisema Kova.
Alisema majambazi hao, wakati wa tukio, walizingirwa na wananchi waliojitolea ambao walikuwa wanawafukuzia kwa pikipiki hatimaye kuwakamata.
Kamishna Kova alisema, baada ya kuzungukwa na wananchi majambazi hao walianza kurusha fedha hizo walizokuwa wamezipora pamoja na mbinu hizo wananchi waliwatupia mawe kwa hasira na kuweza kuwajeruhi vibaya.
Aidha, alisema polisi waliingilia kati na kufanikisha kuwaokoa na pesa taslimu sh. milioni tano ambazo walifanikiwa kumwibia mfanyabiashara huyo.
Hata hivyo, Kova alisema majambazi hao walifariki njiani wakati wakipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu kutokana na majeraha makubwa waliyopata kwa kipigo kutoka kwa wananchi.

No comments:

Post a Comment