16 August 2013

MADUDU ZAIDI AIRPORT DAR



Na Rehema Mohamed
UWANJA wa Ndege wa Kima t a i f a wa J u l i u s Nyerere (JNIA), umeendelea kukabiliwa na kashfa ya kupitisha dawa za kulevya baada ya mkazi wa Dar es Salaam, kukamatwa jana na shehena ya dawa hizo muda mfupi baada ya Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, kufanya ziara uwanjani hapo
.Akizungumza na waandishi Dar es Salaam jana, Dkt. Mwakyembe alimtaja mtu huyo kuwa ni Bw. Jeremia Monyo (39) ambaye ni fundi mbao, mkazi wa Tegeta Mchakani.Alisema kijana huyo mwenye rasta, alikamatwa akiwa na pipi 86 za dawa za kulevya aina ya heroin na misokoto 34 ya bangi akiwa ameiweka katika begi dogo.
"Huyu kijana alikamatwa saa 2:15 usiku kiwanjani hapo baada ya mzigo wake kutiliwa shaka na wakaguzi wa mizigo ambao majina yao ni Grace Jonathan na Crantina Jonathan, waliokuwa na mitambo ya kukagulia.
"Alikuwa na hati ya kusafiria namba AB 202513 akienda nchini Italia kupitia Zurich...nawapongeza hawa wakaguzi waliofanikisha kukamatwa kwake."Nitauagiza uongozi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAAA), uangalie namna ya kuwapandisha vyeo au kuwaongeza mishahara," alisema Dkt. Mwakyembe.
Aliwataka wakaguzi hao, kufanya kazi zao bila woga baada ya kuwataja majina yao hadharani kwani wamefanya kazi nzuri hivyo wanastahili kupongezwa."Sihatarishi maisha yao kwa kutaja majina hadharani, hakuna mwenye mkataba wa kuishi milele na Mungu...hata mimi sitaishi milele hawa wamefanya kazi nzuri wanastahili kupongezwa, kama hupendi joto usiingie jikoni," alisema.
Aliongeza kuwa, baada ya kukamatwa kijana huyo kuanzia sasa watachapisha picha za watu wote ambao watakamatwa uwanjani hapo wakipitisha dawa za kulevya.Dkt. Mwakyembe alisema, pia wataanzisha utaratibu wa kukagua mizigo inayopitishwa katika bandari zilizopo nchini kwa njia ya kisasa zaidi.
Katika hatua nyingine, Dkt. Mwakyembe alisema baada ya ukaguzi wake uwanjani hapo, alibaini tatizo la upitishaji dawa za kulevya katika uwanja huo halitokani na mitambo ya ukaguzi bali watendaji wenyewe waliopewa dhamana.
A l i s e m a s u a l a h i l o atalishughulikia na watendaji wote ambao watabainika kuhusika na upitishaji wa dawa hizo, wataachishwa kazi bila kuoneana haya wala kuwaogopa.
"Kiwanja chetu kina utaratibu mzuri wa kukagua mizingo na vifaa vipo vya kutosha ila tatizo ni watumishi waliopewa dhamana ya kusimamia majukumu, lazima hali hii tuidhibiti kwani kiwanja hiki kinapitisha viongozi wakubwa," alisema.
Aliongeza kuwa, mbali na Watanzania kukamatwa na kilo 120 za dawa hizo nchini Afrika Kusini, taarifa nyingine zinasema kuna Watanzania wengine wawili wamekamatwa HongKong, China ambapo jambo hilo atalizungumzia leo.

3 comments:

  1. Tatizo lilipo ni rushwa bila kutoa mambo haya taendelea.Baadhi ya wafanyakazi hawana kiwango cha elimu kuweza kufanya hapo sijui wamepataje kazi hiyo.Tupo sisi watanzania tulio na elimu ya juu na ujuzi wa Hall ya juu lakini nafasi hizo hatupewi.

    ReplyDelete
  2. kuna vijana wengi tupo magharibi huku na elimu ya kutosha na uchungu wa nchi yetu ,tupewe hata nafasi ya kujitolea hata kwa wiki 2 tukija likizo nyumbani,km ni lugha tunazijua,hatuogopi wageni ila tutaitetea nchi yetu,tupo km nurse,na wataalam wa computer,na biashara ,tunaweza kujitolea pia.na kuongeza camera hata kwenye viungo vya barabara za dar,arusha,na moshi na mwanza wajanja wanakopitia.tushirikisheni mtaona tofauti.

    ReplyDelete
  3. Tatizo nchi yetu inaongozwa kwa mazoea na ndio maana mambo yanenda kienyeji tu.Nchi hii ina vijana wengi tu wenye nia ya kufanya kazi kwa kuwajibika lakini hawapati hizo kazi sababu nafasi zilizopo ni kwa ajili ya wale wanaojuana na wengine hata vigezo hawana.

    ReplyDelete