Na Derick Milton, Simiyu
MA D I W A N I w a Halmashauri ya Wilaya
ya Bariadi wameazimia kusimamisha shughuli za kampuni ya uwekezaji ya Red Hill
Nickel iliyoingia mkataba na Serikali kuchimba madini aina ya Nickel katika
Kata ya Dutwa wilayani humo, kwa kile kinachodaiwa kuwa kampuni hiyo kuanza
shughuli za utafiti wa madini hayo bila ya halmashauri kuhusishwa.
Kampuni
hiyo iliyoingia mkataba na Wizara ya Nishati na Madini kuchimba madini hayo
ilianza shughuli za utafiti wa maeneo yanayomilikiwa na wananchi kwa kuchimba
mchanga na kuacha mashimo, bila ya kulipia ushuru ndani ya halmashauri husika.
Hatua
hiyo ya azimio la kusitisha shughuli zote zinazoendeshwa na kampuni hiyo
ilifikiwa katika kikao cha Baraza la madiwani hao kilichofanyikia katika mjini
humo ili kuweza kupata ufafanuzi juu ya halmashauri itakavyonufaika na
uchimbaji wa madini hayo.
Wakiongea kwa nyakati
tofauti madiwani hao walieleza kuwa mwekezaji huyo amekuwa akialikwa katika
vikao mbalimbali vya halmashauri ili kukutana na madiwani, kwa ajili ya kuweza
kutoa ufafanuzi juu ya halmashauri itakavyonufaika.
Waliongeza kuwa mbali
na kuombwa kila kikao cha baraza kwa mwekezaji huyo kuhudhuria ili kuweza kutoa
fafanuzi juu ya suala hilo, kampuni hiyo imekuwa ikitoa sababu mbalimbali kwa kuandika
barua ya kujulisha kwao kutoshiriki vikao hivyo kwa sababu mbalimbali.
Akitoa ushauri kwa
madiwani hao Mwanasheria wa Halmashauri hiyo, Engelberth Kalekona aliwataka
wadiwani hao kuandika barua kwa Waziri mwenye dhamana ya madini yenye madai
hayo ili kuweza kumsimamisha mwekezaji huyo.
Alisema Halmashauri
haina uwezo wa kuweza kusimamisha shughuli zinazoendelea kufanywa na mwekezaji
huyo, kwa kuwa mkataba wa uchimbaji wa madini hayo uliingiwa baina ya Wizara
husika na mwekezaji na siyo halmashauri na mwekezaji huyo.
Mwenyekiti
wa Halmashauri hiyo, Mabula Magamula aliagiza kuandikwa barua ya kwenda moja
kwa moja katika Wizara ya Nishati na Madini ili kumuomba Waziri kusitisha kazi
hizo hadi kampuni hiyo itakapotoa ufafanuzi wa kina juu ya kunufaika kwa
halmashauri na uchimbaji huo.
No comments:
Post a Comment