27 August 2013

KIKWETE AMWAPISHA JAJI MUTUNGI



Na Penina Malundo
RAIS wa Jakaya Kikwete, jana amemwapisha Msajili Mpya wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji mstaafu Francis Mutungi baada ya aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo, Bw. John Tendwa kustaafu. Ak i z u n g umz a b a a d a y a kuapishwa Ikulu, Dar es Salaam, Jaji Mutungi alisema ingawa kazi hiyo inachangamoto kubwa,
amejipanga kikamilifu kuifanya kwa uadilifu.
Alisema katika utendaji kazi wake, anatarajia kutenda haki na usawa bila ubaguzi wowote. "Mimi bado mgeni katika ofi si hii, sina maneno mengi ila kazi hii ni nzito, nahitaji ushirikiano wa kila Mtanzania," alisema Jaji Mutungi.
 Aliongeza kuwa, baada ya miezi mitatu atazungumza na wananchi kuhusu mikakati yake katika ofi si hiyo. Kwa upande wake, Bw. Tendwa alisema kazi kubwa iliyopo katika Ofi si ya Msajili ni kukuza demokrasia. "Kipindi cha uongozi wangu katika Ofi si ya Msajili nimekabiliana na changamoto nyingi, vyama vya siasa vilikuwa na migongano mingi kwa viongozi wake lakini nilihakikisha vimesimama. "Kustaafu kwangu si mwisho wa maisha yangu bali ni njia moja wapo ya kunifanya niendelee na kazi zangu katika taasisi nyingine za kijamii," alisema

No comments:

Post a Comment