Na John Gagarini, Kibaha
RAIS Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa
mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa mfuko wa Wajasiriamali w a k a t i w a Tama s h
a l a Wajasiriamali wilayani Bagamoyo mkoani Pwani litakalofanyika Septemba 19
mwaka huu
.Mwenyekiti
wa tamasha hilo, Abdul Sharifu alisema kuwa tamasha hilo ambalo litafanyika
kwenye ukumbi wa Chuo Cha Sanaa Bagamoyo (TASUBA).Sharifu alisema kuwa
tamasha hilo litawashirikisha wajasiriamali zaidi ya 500 kutoka kwenye kata 22
za wilaya hiyo ili kuunda chombo cha pamoja kwa lengo la kuboresha shughuli
zao.
Sharifu ambaye pia ni
Meya wa mji wa Bagamoyo alisema kuwa tamasha hilo litaambatana na mafunzo ya
siku tano kwa wajasiriamali hao."Wakufunzi
watatoka kwenye sekta mbalimbali ikiwemo na Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo
(SIDO) ili kuwapatia ujuzi wa kutengeneza bidhaa zao kwa viwango vinavyotakiwa
kwenye soko la ndani na nje ya nchi," alisema Sharifu.
Aidha alisema kuwa
changamoto kubwa aliyoiona kwa wajasiriamali wilayani humo ni ukosefu wa mitaji
pamoja na upatikanaji malighafi na vifaa pamoja na pembejeo kwa wakulima.Aliongeza kuwa
tamasha hilo litawahusisha wajasiriamali
wadogowadogo wakiwemo mama lishe, wachonga vinyago, wafugaji wadogowadogo,
wakulima, wafanyabiashara na vikundi mbalimbali vya uzalishaji mali.
No comments:
Post a Comment