01 August 2013

HARAMBEE KANISANI ZAZIDI KUIBUA MAPYA



Na Suleiman Abeid, Simiyu
MKUU wa Mkoa wa Simiyu, Paschal Mabiti, amelipongeza Kanisa Katoliki Kigango cha Kilole, kwa kumwalika Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta kuongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo na kuwaacha viongozi ambao si waadilifu ambao wangetoa fedha zinazotokana na mikono michafu.Mabiti alitoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa hilo wilayani Busega. Alisema Sitta ni kiongozi mwadilifu asiye na kashfa yoyote serikalini na ni mfano wa kuigwa
. "Napongeza uongozi wa kanisa hili kwa kumchagua Sitta kuongoza harambee hiyo badala ya kuchagua viongozi ambao si waadilifu ambao wangetoa fedha zinazotokana na mikono michafu," alisema.Akitoa historia ya Sitta kwa waumini waliohudhuria harambee hiyo, mkuu huyo alisema mwaka 1977 Sitta akiwa naibu waziri wa mawasiliano nchini ndiye aliyefanikisha uanzishwaji wa vyombo vipya vya umma nchini baada ya kuvunjika kwa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Alisema Sitta ndiye aliyejenga barabara kutoka Morogoro hadi Dodoma kwa kiwango cha lami, daraja la Salander, Shirika la Reli (TRC), Shirika la Ndege (ATC) ikiwemo pia bandari ya Dar es Salaam na kwamba ni miongoni mwa wabunge waliofanikisha kuchaguliwa kwake (Mabiti) kuwa mbunge mwaka 1985.
“Hata daraja la Kirumi kule mkoani Mara, daraja la Salander Dar es Salaam, barabara ya Makambako hadi Songea zote hizi zilijengwa na Sitta, sasa niwaulize hapa katika kipindi chote hicho ni nani miongoni mwenu aliyewahi kusikia huyu bwana akituhumiwa kwa kashfa yoyote ile, asimame hapa ataje,” alihoji Mabiti na kushangiliwa na wananchi.
Alisema kanisa linapochagua mgeni rasmi kuongoza harambee linatakiwa lichague mtu msafi na kwa kuwa kanisa la Mungu halifai kujengwa kutokana na fedha chafu na kwamba Sitta ni miongoni mwa viongozi wasafi na waadilifu nchini hali ambayo ilisababisha hata yeye (Mabiti) kukubali kushiriki katika harambee hiyo.
“Kanisa linapochagua mgeni rasmi kuja kwenye harambee kama hii lisiite kiongozi kama kiongozi, kuna wengine wana fedha haramu ambazo hazifai kujenga kanisa la Mungu, mheshimiwa Sitta ni kiongozi safi na ndiyo maana hata akina sisi (Mabiti) tumekuja, vinginevyo nisingekuja, ningetoa udhuru, lakini niliposikia ni yeye (Sitta) nikaja,” alisema Mabiti.
Kwa upande wake Sitta akizungumza katika harambee hiyo aliwapongeza wananchi wote waliojitokeza katika shughuli hiyo ambapo alisema yeye binafsi ameridhishwa na mwitikio waliouonesha na kufafanua kuwa baadhi ya wenzake ambao wangeshiriki katika harambee hiyo walipata udhuru na kwamba watakwenda kwa wakati wao.
“Wenzangu ambao ningekuja nao hapa leo wamepata udhuru, wengine wako katika ziara ya Rais kule Kagera na mwingine yuko Zimbabwe kufuatilia shughuli za uchaguzi mkuu unaofanyika nchini humo, lakini leo siyo mwisho, huu ni mwanzo, tutakuja tena, naamini tutaendesha harambee babu kubwa, nitamleta na Waziri Mkuu Pinda,” alisema Sitta.
S i t t a a l iwa t a h a d h a r i s h a Watanzania wanaopiga kelele wakilalamikia kutoyaona maisha bora kama walivyoahidiwa na serikali ya CCM kwa kueleza kuwa maisha bora hayawezi kuwadondokea watu wasiojishughulisha na kufanya kazi yoyote ya kuwaingizia kipato.
Kuhusu suala la ufisadi, waziri Sitta alisema Watanzania wanapaswa kujitenga mbali na watuhumiwa wanaobainika kuj ihusishan avitend ovya ufi sadi nakwamb aw apob aadhiyaoambao hivi sasawanahangaikakupitakilakona wakisambaza fedha.
Zaidi ya shilingi milioni 120 zilik usanywa katikaharambeehiyoambayoilikuwa imelenga kuk usany akiasi chash. milioni 270hukuw aziriSitta akichangiash. milioni tatu na mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mabiti aliyechangia sh. milioni moja  

No comments:

Post a Comment