06 August 2013

GAZETI LA MAJIRA LAPONGEZWA MUFINDI


MKURUGENZ I Mt e n d a j i wa H a l m a s h a u r i ya Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Paul Ntimka amelipongeza gazeti la Majira kwa kuandika habari nyingi za maendeleo wilayani Mufindi.Hali ambayo imesababisha wananchi kujua shughuli za maendeleo ambazo zinafanywa na Serikali ya wilaya katika maeneo ya vijijini huku akivitaka vyombo vingine vya habari kuiga mfano wa Majira katika kuandika taarifa za ukweli.

Taarifa ambazo zinalenga maendeleo ambayo Serikali inafanya hususan katika maeneo ya vijijini ikiwemo miradi ya maji, barabara, umeme, kilimo, misitu, afya na ujasiriamali.
A k i z u n g u m z a j a n a kwenye Baraza la Madiwani lililofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, Ntimka alisema gazeti hili ni mfano wa kuigwa hivyo madiwani, maofisa watendaji na wenyeviti wa vijiji wanatakiwa watoe ushirikiano wa kutoa habari.
Alisema kuwa, kumekuwa na tabia ya baadhi ya viongozi kuwakimbia waandishi wa habari wakati wanapofika kuzitafuta habari nzuri na zinazohusu maendeleo.
"Viongozi wa vijiji, madiwani, watendaji wa vijiji, kata na tarafa ninawaomba toeni ushirikiano mkubwa kwa vyombo vya habari, pale ambapo habari katika kijiji chako zinaandikwa kuhusiana na maendeleo ambayo yamefanyika ni sifa kwako wewe kiongozi, Serikali na wananchi wanatambua kuwa kumbe Serikali yao inawafanyia nini na siyo kuwakimbia, kwa nini mnawaogopa waandishi wa habari, wana malengo mazuri na taifa letu," alifafanua Mkurugenzi huyo.
Aliongeza kuwa, gazeti la Majira katika kuandika habari zake wanahakikisha wanajiridhisha katika vyanzo vyote vya habari wakiwemo wananchi, viongozi ngazi za vijijini, kata, tarafa na wilaya suala ambalo limesababisha k u w a n a u m o j a n a mshikamano kiutendaji kwa kuwa na mfumo wa habari zenye mtiririko sahihi kutoka ngazi za chini hadi juu.
K w a u p a n d e w a k e Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, Peter Tweve aliunga mkono kauli ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, Paul Ntimka na kuongeza kuwa ili vijiji, kata, tarafa na wilaya iweze kutambulika m a t a t i z o y a k e n a maendeleo yake kunatakiwa kuwepo ushirikiano mkubwa baina ya viongozi wa ngazi zote.
Sambamba na vyombo vya habari na siyo kukimbiana na kushindwa kupeana habari.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa, miradi mingi ambayo imekuwa ikifanywa na Serikali katika maeneo ya vijijini inatakiwa ijulikane na siyo kuiweka kiusiri ambapo alisema kuwa, gazeti la Majira limekuwa likitoa habari za maendeleo na kufukua habari zote zenye kuwatofautisha wananchi na Serikali ili kuhakikisha kunajengwa umoja makini kati ya wananchi na Serikali yao.
Alisema kuwa, katika ulimwengu unavyokwenda k w a s a s a w a n a n c h i wanatakiwa waambiwe wazi kuhusiana na maendeleo a m b a y o s e r i k a l i y a o inawafanyia na siyo kuficha ficha suala ambalo wananchi baadaye wanaweza kuanza kuhoji kulikoni huku vyombo vya habari vikifuatilia mashaka hayo wakati kama ushirikiano ungekuwepo mambo yangeenda vizuri.

No comments:

Post a Comment