15 August 2013

CHEKA KUZIPIGA NA MMAREKANI AGOSTI 30



Na Ester Maongezi
KAMPUNI ya 'Hall of Sam B and Promotion Companies' wameandaa pambano la ngumi la dunia uzito wa kati (WBF) kati ya bingwa wa bara la Afrika, Francis Cheka na Philly William wa nchini Marekani litakalofanyika Agosti 30, katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam

Akizungumza Dar es Salaam jana Mratibu wa pambano hilo, Jay Msangi, alisema kuwa pambano hilo litakuwa ni la raundi 12 na uzito wa kilo 76 pamoja na kusindikizwa na mapambano mengine manne.Msangi alisema mbali na pambano hilo pia kutakuwa na mapambano ya utangulizi kati ya Mada Maugo pamoja na Thomas Mashali pambano la raundi 12.
Msangi alisema aliamua kuwakutanisha Maugo na Mashali katika pambano la utangulizi ili kuweza kuvunja majigambo kati ya mabondia hao wawili."Unajua Maugo na Mashali kila mmoja anajigamba kuwa yeye ni bondia bora baada ya Cheka, yaani baada ya Cheka kushika nafasi ya kwanza ya ubingwa wa Afrika wa pili ni wao hivyo swali la jibu hilo nani ni nani litapatikana siku hiyo," alisema Msangi
Pia kutakuwa na pambano la uzito wa juu kati ya Alphonce Mchumia na Deandre McCole wa Marekani, Ibrahimu Classic wa Tanzania atakipiga na Simba wa Tundani wote wa Tanzania na kutakuwa na pambano kati ya Cosmas Cheka na Allan Kamote.
Msangi alisema mpambano huo utukuwa wa kihistoria nchini, hivyo amewataka mashabiki wa mchezo wa ngumi nchini kujitokeza kwa wingi ili kujionea ushindani utakaojitokeza.Viingilio katika pambano hilo litakuwa viti maalum ni sh.150,000, VIP gold 50,000 na 20,000 kwa viti vya kawaida.Tiketi zitaanza kuuzwa kuanzia keshokutwa huku mgeni rasmi katika pambano hilo atakuwa Frankois Botha bingwa mara mbili wa Dunia

No comments:

Post a Comment