07 August 2013

CCK YAINGILIA MGOGORO WA RWANDA


 Na Goodluck Hongo
CHAMA cha Kijamii (CCK) kimemtaka Rais Jakaya Kikwete na washauri wake kutafuta njia za kidiplomasia za kuzungumza na Rais wa Rwanda, Paul Kagame ili kutafuta suluhisho la mivutano inayoendelea kwa sasa kati ya pande mbili.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Mwenyekiti Taifa wa chama hicho, Constantine Akitanda alisema kuwa kwa sasa kumekuwa na ushabiki mkubwa juu ya uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda hivyo ni vema zikatumika njia za kidiplomasia ili kutatua sababu za kurushiana maneno baina nchi yetu na Rwanda.
Alisema, kwa sasa baadhi ya watu wako tayari na wameanza kushabikia vita au kutafuta suluhu kwa nguvu za kijeshi huku wengine wakitamba kuwa tunaweza kuichakaza Rwanda kama tulivyofanya kwa Idi Amin.
Alisema, mawazo ya namna hiyo ni ya hatari na inawezekana yanatolewa pasipo kufikiria ambapo wale wanaotoa kauli hizo ni lazima watambue kuwa vita si kitu kizuri kwani majeraha yake yanadumu kwa vizazi na vizazi.
"Kwa wale ambao wamefika K a g e r a h a s a m a e n e o yaliyoathirika na vita wanaweza kuona makovu yaliyobakia miaka zaidi ya 30, baada ya vita sasa tunawasihi viongozi wetu na vyombo vya habari kuepuka kuchochea kauli za vita na uhasama kwa sababu tunaamini tu kuwa nchi yetu ina uwezo wa kuipiga Rwanda na kusahau kabisa kuwa vita ni sehemu mbili kama vita ya Uganda ilivyotufundisha," alisema Akitanda

No comments:

Post a Comment