Na Mwandishi Wetu
JUMLA ya wanamichezo 25 wamechukua fomu
kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania
(TFF) unaotarajiwa kufanyika Oktoba 27, mwaka huu.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na
Ofisa Habari wa TFF Boniface Wambura ilieleza kuwa fomu hizo zilianza kutolewa
Agosti 16 mwaka huu ambapo wawili wamechukua nafasi ya Rais.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa wadau
wengine wawili wamechukua fomu za Makamu wa Rais wakati waliobaki wanaomba
ujumbe wa Kamati ya Utendaji wakiwakilisha kanda mbalimbali.Waliochukua fomu za kuomba kuteuliwa
kuwa wagombea urais ni Jamal Malinzi na Omari Musa Nkwarulo wakati umakamu wa
rais hadi sasa umewavutia Wallace Karia na Ramadhan Nassib.
Waliochukua fomu za ujumbe ni Athuman
Kambi, Charles Komba, Davis Mosha, Elias Mwanjala, Eliud Mvella, Epaphra Swai,
Farid Nahdi, Hussein Mwamba, Jumbe Magati, Kamwanga Tambwe na Khalid Mohamed.
Wengine ni Muhsin Balhabou, Omari
Abdulkadir, Omari Walii, Samwel Nyalla, Shaffih Dauda, Stanley Lugenge, Twahir
Njoki, Vedastus Lufano, Venance Mwamoto na Wilfred Kidao.Kwa upande wa Bodi ya Ligi Kuu
aliyechukua fomu mpaka sasa ni Hamad Yahya anayeomba kuteuliwa kugombea nafasi
ya uenyekiti.
Fomu za maombi pia zinapatikana kupitia tovuti
ya TFF ambayo ni www.tff.or.tz mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni saa 10
kamili jioni ya Agosti 20 mwaka huu
No comments:
Post a Comment