Na Amina Athumani
NAHODHA wa timu ya Yanga Nadiri Haroub
'Canavaro' amewaasa wachezaji wenzake wa klabu yake na ya Simba kutoamini
ushirikina katika soka, lakini uwezo wao na juhudi zao ndiyo zitasaidia timu
zao kufanya vyema hasa katika Ligi Kuu Tanzania bara.
Canavaro
alisema jana wakati wa semina elekezi kwa klabu zinazoshiriki Ligi Kuu na
Daraja la Kwanza iliyoandaliwa na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es
Salaam (DRFA), kwa timu za mkoa huu, ambapo semina hiyo ililenga kutoa mafunzo
ya sheria 17 za soka, jinsi ya kuripoti habari za klabu na Kamati ya Ufundi.
Alisema masuala ya ushirikina waziachie
kamati za ufundi wao, wajikite katika kuhakikisha wanajituma na kuzingatia
mafunzo ya walimu ili kuweza kuhakikisha wanafanya vyema katika timu zao na sio
kuingilia masuala yasiyowafaa.
"Kama kuna masuala ya ndumba yapo
na yataendelea kuwepo kwani yameshajengeka katika fikra za watu, lakini sisi
wachezaji hasa Yanga na Simba tuzingatie mazoezi na kujituma, hayo masuala
mengine tuwaachie wao wanaofanya," alisema.
Alisema kwa upande wa Yanga wao hawajashuhudia mambo
hayo na wao kinachowasaidia kufanya vizuri ni mazoezi na kujituma na ndiyo
maana timu yao imekuwa ikifanya vizuri siku zote na viongozi hawajihusishi
katika masuala hayo
No comments:
Post a Comment