Na Amina Athumani
WA N A R I A D H A w a Tanzania waliokwenda kushiriki mashindano ya
Dunia kwa upande wa mbio ndefu za Marathon,
wameshindwa kufanya vizuri katika michuano hiyo, huku mwanariadha Fautine Mussa
akishika nafasi ya 34 na Msenduki Mohamed kuambulia nafasi ya 39
Mashindano hayo
yalifanyika katika uwanja wa Luzhniki Stadium katika jiji la Moscow
nchini Urusi ambapo yalikuwa na mbio mbalimbali kuanzia mita 100 hadi mbio
ndefu za Marathon.
Mussa alimaliza mbio hizo akitumia muda
wa saa 2:20:51 wakati Msenduki akimaliza kwa kutumia muda wa saa 2:24:20.
Michuano hiyo iliyoshirikisha
wanariadha kutoka nchi mbalimbali, ilikuwa na upinzani mkali huku Uganda
iking'ara kwa kutwaa medali ya dhahabu katika mbio ndefu.
Kutokana na matokeo hayo Tanzania bado
imeendelea kufanya vibaya katika michezo ya Kimataifa ambapo mbali na
mashindano hayo ya Dunia Mussa na Msenduki pia hawakuweza kufanya vizuri katika
mbio hizo katika michezo ya Olimpiki iliyofanyika mwaka jana.
No comments:
Post a Comment