Na Elizabeth Mayemba
MSHAMBULIAJI wa Mtibwa Sugar ya
Morogoro, Hussein Javu tayari amemwaga wino katika klabu kongwe nchini ya Yanga
na moja kwa moja jana alianza mazoezi na wenzake Uwanja wa Loyola Mabibo, Dar es Salaam.Javu amesaini mkataba wa miaka miwili
kuichezea klabu hiyo ambao pia ni mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya
Usajili ya klabu hiyo, Abdallah Bin Kleb alisema wamemalizana na Javu pamoja na
klabu yake ya Mtibwa na sasa ni mchezaji mpya wa Jangwani."Tumemsainisha Javu miaka miwili,
tumemalizana naye yeye na klabu yake," alisema Bin Kleb.
Klabu hiyo imeamua kumsajili Javu ili
kuimarisha safu ya ushambuliaji baada ya Kocha Mkuu wa timu hiyo kumfungashia
virago Mnigeria Ogbu Brendan Chukwudi.
Pia Javu aliwahi kuwa mchezaji wa timu
ya taifa, Taifa Stars wakati timu hiyo ilipokuwa ikinolewa na Mbrazil Marcio Maximo.Kusajiliwa kwa Javu, kunaongeza
ushindani katika safu ya ushambuliaji ya timu hiyo kwani sasa inakuwa na watu
wanne, wengine ni Jerry Tegete, Didier Kavumbangu na Shaaban Kondo.
Javu
ni mchjezaji wa tatu kutoka katika timu yake ya Mtibwa kusajiliwa kwani tayari
Yanga ilimnasa beki, Rajab Zahir huku mahasimu wao Simba wakimsajili Issa
Rashid 'Baba Ubaya' na Shaaban Kisiga alijiondoa mwenyewe baada ya kutofautiana
na kocha wake.
No comments:
Post a Comment