26 July 2013

WIZI MINARA YA SIMU KIKOSI KAZI CHAUNDWA



Na Stella Aron
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), limeunda kikosi kazi maalumu (Special Task Force) kwa ajili ya uchunguzi juu ya tuhuma za wizi wa umeme kwenye minara ya simu nchini.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari jana Dar es Salaam na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, TANESCO imesema kuwa tayari kikosi kazi hicho kimeanza kazi kupitia minara yote ya makampuni ya simu nchini
. Alisema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa kuna upotevu wa mapato ya shirika katika baadhi ya minara hiyo.Taarifa hiyo imesema kuwa kutokana na taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari kuhusu upotevu wa umeme kwenye minara ya simu unafuatiliwa kwa kina na kufanya ukaguzi kwenye minara yote ili kubaini ukweli kuhusu hujuma hizo.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa uongozi wa shirika unaahidi kuwa uchunguzi wa tuhuma hizo utakuwa huru, wa wazi na usiomuonea mtu au kampuniyoyote . Ilisisitizwa ku wa u chunguzihuo utaf anyikakitaalamunakwaumakini mkubwa.Ilieleza kuwa uchunguzi utakapokamilika, kampuni za simu zitakazobainika kuiba umeme zitalazimika kulipia kiasi chote cha umeme uliotumika bila kulipiwa pamoja na riba kwa kipindi chote.
Sakata la hujuma kwenye minara liliibuliwa na Majira wiki iliyopita wakati maofisa wa TANESCO walipofanya operesheni ya kukagua minara wilayani Ilala.Wakati ukaguzi huo ukifanyika ili kubaini hujuma baadhi ya waandishi wa habari walifika, lakini mmoja wa maofisa wa TANESCO aliwazuia kwa madai kuwa wamepata maelekezo kuwa hawatakiwi kuwepo.
Baada ya kufanyika ukaguzi kwenye minara miwili, walibaini kila mnara kuwa na mita mbili. Wakati huo huo, habari za uhakika ambazo Majira imepata zimeeleza kuwa wafanyakazi wa TANESCO walioshiriki operesheni ya kuibua wizi huo kupitia kwenye minara wametishiwa kufukuzwa kazi.
Akizungumza na Majira kwa njia ya simu hivi karibuni jana, Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alisema Wizara imeiagiza bodi na menejimenti kufuatilia na kutoa taarifa serikalini."Tumeielekeza bodi ifuatilie suala hilo na baadaye itatupa majibu," alisema Profesa Muhongo

No comments:

Post a Comment