Na Heri Shaaban
WA T A B I B U
wameiomba Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Mamlaka ya Chakula na Dawa
Tanzania (TFDA) kufanya uchunguzi upya na wa kina wa mafuta ya karafuu,
alizeti, mwarobaini na mlonge ili kuondokana na hofu iliyopo kwa jamii. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi
wa Kituo cha Tiba, Lishe na Ushauri na Vipodozi Asili cha Tabata, Dkt. Othman
Shem alisema sababu ya ombi hilo ni kutokana na mkanganyiko wa mafuta ya ubuyu
kuwa si salama kwa matumizi
. Alisema kuwa hatua hiyo inatokana na taarifa ya TFDA kwa umma ya
kuzuia mafuta ya ubuyu kwa madai kuwa yana madhara kiafya wakati yametumika
zaidi ya miaka saba. A l i s ema k u w a i l i kuondokana na mkanganyiko huo ni vizuri
Wizara ya Afya, TFDA na Taasisi ya Utafiti Tanzania (NIMRI) kuyafanyia
uchunguzi mafuta hayo na kutoa taarifa sahihi kwa umma.
"Matumizi ya mafuta ya ubuyu yameanza kutumika zaidi ya miaka
saba iliyopita na jamii na ulimwengu wanayatumia katika kipindi hicho
hayakuonekana kama yana madhara kwa binadamu kwanini leo serikali izinduke
usingizini na kuona hayafai," alihoji Shem.
A l i s e m a k a m a imegundulika mafuta ya ubuyu si salama
kutokana na uchunguzi pia ni vizuri sasa wakafanya uchunguzi wa mafuta ya
karafuu, mlonge, alizeti na mwarobaini ambavyo vimetumika muda mrefu. Pia wameomba kuzingatia suala la vifaa kwani kuna uwezekano wa
vifaa vya awali kuwa na kasoro hivyo ni vizuri mafuta ya ubuyu yakapimwa upya.
" H u e n d a m a f u t a waliyotumia TFDA kuyapima labda
yalikuwa yamevunda ndio maana wamegundua kutofaa kiafya lakini nchi zaidi ya
100 mpaka sasa wanatumia mafuta hayo," alisema.. Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya, Sefu Rashidi alisema taarifa
imechelewa kutolewa kwa umma kutokana na kuyafanyia uchunguzi taratibu na kuonekana
kuwa na madhara ya kansa.
No comments:
Post a Comment