Na Suleiman Abeid, Simiyu
WAKAZI wa Wilaya ya
Maswa Mkoa wa Simiyu wameelezea wasiwasi wao kuhusiana na changamoto nyingi
zilizomo ndani ya rasimu ya katiba na kwamba zinapaswa kupatiwa ufumbuzi wa
kina kabla ya kuandikwa rasmi kuwa Katiba Mpya nchini.
Wakitoa maoni yao
katika mdahalo ulioandaliwa na Muungano wa asasi za kiraia wilayani Maswa
(MASWANGONET) kwa ufadhili wa The Foundation For Civil Society uliofanyika juzi
wakazi hao walisema yapo maeneo mengi ambayo yanapaswa kufanyiwa marekebisho
kabla ya rasimu hiyo kufikishwa katika bunge la katiba.
Baadhi ya eneo lililotajwa kuwa na changamoto nyingi ni suala la
muundo wa Muungano iwapo muundo wa Serikali tatu utakubalika na kwamba
haieleweki ni jinsi gani itifaki ya marais wa Tanzania Bara, Serikali ya Zanzibar na yule ya
Muungano itakavyoweza kutekelezwa.
Walisema rasimu ya hivi sasa haielezi kwa kina suala la itifaki za
watakaokuwa marais chini ya muundo wa Serikali tatu na kuhoji iwapo Rais wa
Muungano amehudhuria sherehe ya kitaifa katika nchi moja washiriki wa muungano
ni rais yupi anayepaswa kutangulia katika uwanja wa sherehe na kupigia mizinga
ya heshima kama ikibidi kupigwa.
"Kwa kweli rasimu yetu bado ina maeneo mengi sana
yanayopaswa kufanyiwa marekebisho na kupatiwa ufafanuzi wa kina, binafsi
ninapata wasiwasi sana katika suala zima la
itifaki ya marais wetu itakuwaje, sasa lifanyiwe kazi kwanza suala hilo ndipo tutoe maoni
yetu."
"Mfano ni hali halisi inavyotokea kule visiwani wakati Rais
wa Muungano anapokaribishwa katika sherehe mbalimbali za kitaifa mfano sherehe
za mapinduzi, tunaona yeye ndiye anayetanguliwa uwanjani, kisha mwisho ndipo
anaingia Rais wa Serikali ya Mapinduzi, hapa kuna mkanganyiko, kwa kawaida Rais
wa Muungano ndiye anapaswa kuingia mwisho," alieleza Ezekiel Kassanga.
Hata hivyo, washiriki wa mdahalo huo walikubaliana kuwepo kwa
muundo wa serikali tatu nchini na pia kushauri kutumika kwa jina la Serikali ya
watu wa Tanganyika badala ya Tanzania bara na kwamba kutotambuliwa kwa
Tanganyika kutasababisha kupotea kwa jina hilo ambalo ni moja ya washiriki wa
muungano huo.
Mbali ya kupotea kwa jina hilo pia
washiriki hao walionesha wasiwasi kwamba kutamkwa kwa neno Tanzania Bara
inaweza kusababisha kutokea kwa mgogoro mkubwa siku zijazo kwa baadhi ya maeneo
ya Tanganyika ambayo ni
visiwa kuamua kujitenga kwa vile hayatajwi ndani ya katiba kuwa ni sehemu ya Tanganyika
kwa kweli wananchi tuliowengi hatutaipigia kura ya maoni katiba mpya endapo suala la serikali tatu kutokuwepo.Hakuna asiyefahamu urasimu uliojaa kwenye muungano wa sasa ambapo nchi moja imekuwa ikikandamizwa kwa muda mrefu.Wanzibari watajitenga tu.......
ReplyDelete