05 July 2013

WANANCHI WAHIMIZWA KUFUGA NYUKI


Na Esther Macha, Mbeya
SERIKALI mkoani Mbeya imewaagiza viongozi wa ngazi za vijiji na kata kutoa elimu kwa wananchi ya ufugaji nyuki ili kuweza kujiongezea kipata kitokanacho na asali ili kujikwamua kiuchumi kutokana na mradi huo kutogharimu fedha nyingi.
Mwito huo ulitolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dkt. Norman Sigala wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Serikali za Mitaa yaliyofanyika katika Kata ya Swaya jijini humo ambapo kauli mbiu ya mwaka ni amani, uadilifu, uwajibikaji ni nyenzo muhimu katika mchakato wa katiba mpya na ustawi wa Serikali za Mitaa.

Alisema kuwa urinaji wa asali hauhitaji pembejeo za kilimo bali ni maandalizi ya kuwepo na mizinga na kwamba kwa kipindi hiki zao hilo limekuwa na faida kubwa ambapo kuna uwezo wa kumwingizia mrinaji zaidi ya shilingi 250,000 kwa mzinga mmoja.
"Ndugu zangu wananchi miradi ni mingi ya kujikwamua kiuchumi na si kutegemea kilimo pekee na kwamba ufikie wakati sasa kuamka na kujikita katika ufugaji wa nyuki na Serikali itakuwa bega kwa bega na nyinyi hususan kuwafikishia wataalam wa ufugaji wa nyuki," alisema.
Aidha Sigala alionya viongozi wa ngazi za vijiji na kata kutobweteka maofisini na badala yake kujikita katika kuhamasisha wananchi katika shughuli mbalimbali za ukuaji wa uchumi kwa mtu mmoja au vikundi kwa kuanzisha miradi endelevu itakayosaidia kuwaongezea kipato hususan miradi ya maendeleoi ya kijiji.
"Viongozi ni wakati wa kutambua nini uhitaji wa jamii katika maeneo yenu na si kubweteka bali ni kuhakikisha wa n a c h i wa n a n u f a i k a na miradi mbalimbali ya maendeleo," alisema.

No comments:

Post a Comment