Na Mwandi
shi We tu, Morogoro
WAKULIMA nchini wamependekeza k u w a p
o k w a k i p e n g e l e k i n a c h o h u s u h a k i z a wakulima katika
Rasimu ya Katiba. Ma
p e n d e k e z o h a y o yalitolewa mjini Morogoro jana na mkulima kutoka
mkoani Kilimanjaro, Freddy Nyakaka wakati akichangia mada katika Mkutano Mkuu
wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA)
. Alisema,
katika rasimu ya katiba iliyopo sura ya nne sehemu ya kwanza katika kipengele
cha haki za binadamu, rasimu imetambua haki za makundi mbalimbali, lakini
haijatambua haki za mkulima mdogo.Ma
p e n d e k e z o h a y o yaliungwa mkono na wajumbe wote waliohudhuria mkutano
huo. Akijibu
hoja hiyo, mtoa mada, Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu
(LHRC), Anord Sungusia, aliwashauri wakulima kuisoma rasimu ya katiba na
kuielewa ili waweze kuijadili, ili kuwasilisha mapendekezo yao kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
"Ni
vyema mtumie fursa hii ya kutoa maoni kwenye rasimu ya katiba, ili haki za
wakulima zitambuliwe kikatiba," alisema. Aliwataka
kutumia fursa hiyo ili kuondoa uonevu na dhuluma kwa wakulima ambayo imekuwapo
kwa miaka mingi nchini.
Alisema wakulima ni
waathirika wakubwa wa haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni pamoja na haki
ya kumiliki mali.Alisema ingawa haki
hazibagui, lakini kuna tofauti kubwa za huduma za jamii katika maeneo ya mijini
na vijijini ambako asilimia 80 ya wananchi wanaishi huko.
Mwanasheria huyo
alisema ingawa haki za binadamu zimeainishwa katika katiba iliyopo, lakini
hakuna nia ya dhati ya kuzilinda haki hizo.Alishauri wakulima kwenda Mahakama Kuu wanapobaini haki zao z i n a v u
n jwa , i n g awa mahakama hizo zipo katika mikoa 11 nchi nzima.
No comments:
Post a Comment