25 July 2013

WAKULIMA WADAI KIPENGELE CHAO RASIMU YA KATIBA



 Na Mwandi shi We tu, Morogoro
WAKULIMA nchini wamependekeza k u w a p o k w a k i p e n g e l e k i n a c h o h u s u h a k i z a wakulima katika Rasimu ya Katiba. Ma p e n d e k e z o h a y o yalitolewa mjini Morogoro jana na mkulima kutoka mkoani Kilimanjaro, Freddy Nyakaka wakati akichangia mada katika Mkutano Mkuu wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA)
. Alisema, katika rasimu ya katiba iliyopo sura ya nne sehemu ya kwanza katika kipengele cha haki za binadamu, rasimu imetambua haki za makundi mbalimbali, lakini haijatambua haki za mkulima mdogo.Ma p e n d e k e z o h a y o yaliungwa mkono na wajumbe wote waliohudhuria mkutano huo. Akijibu hoja hiyo, mtoa mada, Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anord Sungusia, aliwashauri wakulima kuisoma rasimu ya katiba na kuielewa ili waweze kuijadili, ili kuwasilisha mapendekezo yao kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
"Ni vyema mtumie fursa hii ya kutoa maoni kwenye rasimu ya katiba, ili haki za wakulima zitambuliwe kikatiba," alisema. Aliwataka kutumia fursa hiyo ili kuondoa uonevu na dhuluma kwa wakulima ambayo imekuwapo kwa miaka mingi nchini.
Alisema wakulima ni waathirika wakubwa wa haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni pamoja na haki ya kumiliki mali.Alisema ingawa haki hazibagui, lakini kuna tofauti kubwa za huduma za jamii katika maeneo ya mijini na vijijini ambako asilimia 80 ya wananchi wanaishi huko.
Mwanasheria huyo alisema ingawa haki za binadamu zimeainishwa katika katiba iliyopo, lakini hakuna nia ya dhati ya kuzilinda haki hizo.Alishauri wakulima kwenda Mahakama Kuu wanapobaini haki zao z i n a v u n jwa , i n g awa mahakama hizo zipo katika mikoa 11 nchi nzima.  

No comments:

Post a Comment