Na Goodluck
Hongo
AGIZO l a Wa z i r i wa Uj e n z i Dk t
. John Magufuli la kujengwa Barabara ya Jangwani-Kigogo jijini Dar es Salaam
litaanza kutekelezwa kuanzia Agosti 6 mwaka huu licha ya kuwepo kwa kesi
mahakamani.Kesi
ambayo ilifunguliwa na wamiliki wa nyumba wapatao sita katika eneo hilo
. A
k i z u n g u m z a n a mwandishi wa habari hizi jana jijini Dar es Salaam,
Mkurungenzi wa Kampuni ya Heri Sigh tawi la Dar es Salaam ambayo ndiyo ilipata
tenda ya ujenzi wa barabara hiyo, Jospal Sigh alisema ujenzi wa kipande hicho
kilichobaki kitaanza kujengwa rasmi mwezi huo.
Awali
Waziri wa Ujenzi Dkt.Magufuli alifanya ziara katika Mkoa wa Dar es Salaam kukagua miradi mbalimbali ya
maendeleo ikiwemo Barabara ya Jangwani hadi Ubungo ambapo licha ya kukamilika
sehemu kubwa ya barabara hiyo lakini hakukuwa na lami katika kipande cha
kuanzia Jangwani hadi Njiapanda ya Daraja kuelekea Kigogo.
Baada
ya kukagua barabara hiyo, Waziri Dkt. Magufuli ndipo alipotaka kujua sababu za
kushindikana kukamilika kwa barabara hiyo na mkandarasi kukaa eneo la mradi kwa
zaidi ya miaka miwili bila kazi.Akitoa
maelezo mbele ya Waziri Magufuli mhandisi mshauri wa kampuni hiyo, Musa Ally
alisema sababu za kushindwa kumalizika kwa kipande hicho ni kutokana na
wananchi sita kufungua kesi mahakamani hivyo hadi kesi hiyo itakapokwisha ndipo
wataendelea na ujenzi wa kipande hicho.
B
a a d a y a k u p a t a maelezo hayo ndipo Waziri Ma g u f u l i a l i p o i a
g i z a kampuni hiyo kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo kama ulivyopangwa
lakini wasibomoe nyumba hizo hata kama lami
itapita pembeni mwa nyumba hizo
"Fidia
wamechukua lakini hapo hapo wamefungua tena kesi mahakamani na ujenzi ulitakiwa
kukamilika siku nyingi zilizopita sasa Watanzania wajue kuwa wanaochelewesha
maendeleo ni baadhi ya watu wachache kwani fedha zipo za utekelezaji wa miradi
hiyo, nakuagiza mkandarasi ujenge barabara hii mara moja hata kama lami itapita
pembeni mwa nyumba hizo wewe weka lami, lakini usibomoe nyumba hata moja na pia
mtendaji mkuu wa TANROADS nakuagiza ukafungue kesi kwa watu hawa kwa kuitia
hasara serikali kwani hilo linawezekana,"alisema Dkt. Magufuli.
Katika ziara hiyo
Dkt. Magufuli alikagua barabara zote zinazojengwa Wilaya tatu za Mkoa wa Dar es Salaam ikiwemo
mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi wa (DART).
No comments:
Post a Comment