. Na Theophan Ng'itu
MTU mmoja amefariki dunia papo hapo mara baada ya kugongwa na gari
katika Barabara ya Nyerere eneo la Panasonic Wilaya ya Temeke jijini Dar es
Salaam. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Engelbert
Kiondo
alisema kuwa mtu huyo mwanaume ambaye jina lake halikufahamika anayekadiriwa
kuwa na umri wa miaka 45-50 aligongwa na gari lenye namba T 288 AZB aina ya
Nisani Civilian Min-Bus.
Kiondo
alisema kuwa, gari hilo
lilikuwa likiendeshwa na Abraham Said (39) mkazi wa Tandika mji mpya, ambapo
alimgonga mtu huyo aliyekuwa akivuka barabara na maiti imehifadhiwa katika
Hospitali ya Temeke na dereva anashikiliwa na Jeshi la Polisi.
No comments:
Post a Comment