03 July 2013

WAKAZI ILALA WADAIWA KUZEMBEA MATIBABU


Na Heri Shaaban
IMEELEZWA kuwa wananchi wa Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam
wengi wanachelewa kupata huduma za afya mapema hadi wanazidiwa
ndipo wanakumbuka kupelekwa vituo vya afya.
Hayo yalisemwa jana na Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo, Dkt.
Asha Mahita wakati wa uzinduzi wa zoezi la kampeni la kutoa huduma
za afya kwa uwiano katika jamii Kata ya Gongolamboto.

Dkt. Mahita alisema, huduma hizo za kiafya ni muhimu katika kusaidia
makundi maalumu ya watoto na wajawazito, wazee na walemavu ndani
ya manispaa hiyo ili kukabiliana na changamoto hizo.
Kwa upande wake Meya wa Manispaa hiyo, Jerry Silaa alisema
wataalamu wanaeleza matatizo mengi ya kiafya hasa magonjwa
yanayosumbua wananchi wengi yanatokana na uchafuzi wa mazingira na
matumizi ya maji yasio salama.
Hata hivyo, aliwataka wananchi wake watumie utaratibu huo wa kupata
huduma za uwiano bila malipo kwani ni muhimu na utawasaidia watu
wenye kipato cha chini, wasio na uwezo kufuata huduma hiyo karibu na
makazi yao.

No comments:

Post a Comment