05 July 2013

WAJASIRIAMALI WASHINDWA UBUNIFU KWA KUKOSA MAFUNZO


 IMEELEZWA kuwa asilimia kubwa ya wajasiriamali nchini hawashiriki mafunzo ya ujasiriamali hali inayopelekea wajasiriamali wengi kukosa ubunifu zaidi katika shughuli zao, anaripoti Penina Malundo na Jazila Mrutu.
Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na mtafiti wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Utafiti wa Kisera katika Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (STIPRO), Bw. Musambya Mutambala wakati akiwasilisha mada mbele ya wadau wajasiriamari.
Bw. Mutambala alisema kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuwahamasisha wafanyabiashara wa d o g o wa d o g o k a t i k a kuwaendeleza kupanua fikra zao ili waweze kukuza fikra zao katika kuongeza ujuzi.

“Wajasiriamali wengi hawapo tayari kupata mafunzo ya ujasiriamali sijajua ni kwa sababu gani kwani tunawahamasisha kila siku juu ya ushiriki wao katika mafunzo hayo kwani yanawapa fursa ya kuongeza ujuzi katika shughuli zao,”alisema Mutambala.
Ai d h a a l i s ema k a t i k a k u f a n y a u t a f i t i w a k e aligundua kuna changamoto kubwa wanayokabiliana nayo wajasiriamali wadogo wadogo ni pamoja na kukosa vitendea kazi hivyo ameiomba Serikali kuwasaidia wajasiriamali hao kuweza kujikimu katika mahitaji yao.
“Katika utafiti nilioufanya nimegundua kuwa wajasiriamali wengi wanashindwa kufanya vizuri sababu ya vitendea kazi vyao vinakuwa vibovu na muda mwingi vinakuwa vimepitwa na wakati hali inayopelekea vitu vyao kutokuwa vizuri,” alisema.

No comments:

Post a Comment