Rehema Maigala na
Rachel Balama
MENEJA wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF kanda ya kaskazini
Amina Kassim, amewataka waajiri ambao wamejiunga na mfuko huo kuwasilisha mafao
yao kwa wakati ili kuondoa usumbufu wa kufuatilia michango hiyo.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam katika maonyesho
ya 37 ya Kimataifa ya Biashara, Kassim amesema kama michango hiyo itawasilishwa
kwa wakati itasaidia wanachama kulipwa mafao yao mapema mara baada ya kustaafu.
Alisema kuwa katika kuboresha huduma kwa wanachama wao
LAPF ina mpango wa kuanzisha fao la elimu kwa lengo la kuwawezesha wanachama
pamoja na familia zao.
"Tangu
kuanzishwa kwa mfuko huu wa pensheni, tunatoa mafao sita ikiwa ni pamoja na
msaada wa mazishi, ambapo sisi kama viongozi wa LAPF tumeamua kuanzisha fao
jipya la elimu ambalo litamsaidia mwanachama pamoja na watoto wao,"
alisema Kassim.
Alisema
kuwa lengo la kushiriki katika maonyesho hayo ni kutoa elimu kwa wanachama
pamoja na kuelezea mafanikio waliyoyapata tangu kuanzishwa kwa mfuko huo.
A k i e l
e z e a c h a n g amo t o zinazowakabili ni pamoja na wigo mfinyu kwa wanachama
kujiunga na mfuko wa pensheni kutokana na uelewa mdogo.
Alisema LAPF imekuwa ikitoa riba nafuu na rahisi
kwa wanachama wake hali ambayo imesababisha idadi ya wanachama kuongezeka siku
hadi siku
No comments:
Post a Comment