26 July 2013

UBAKAJI BADO NI TISHIO NCHINI



 Na Darlin Said
CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) kimesema kushamiri kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia katika jamii ya Watanzania hasa ubakaji bado ni tatizo linalohitaji nguvu ya pamoja kulitokomeza. Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi Mtendaji wa chama hicho, Valerie Msoka alipokuwa akizindua ripoti ya utafiti wa unyanyasaji wa kijinsia uliofanyika Aprili mwaka huu katika wilaya 10 za Tanzania bara na Zanzibar.

Msoka alisema kwa mujibu wa utafiti huo imeonekana licha ya vitendo hivyo kuendelea kuwepo, waathirika ambao ni wanawake na wasichana wengi wao hawatoi taarifa kwa mamlaka husika ili hatua kali zichukuliwe dhidi ya wahalifu. Alisema tabia ya kutotoa taarifa inasababishwa na mila na desturi zilizowazunguka, hivyo alitoa wito kwa jamii kuachana na utamaduni wa kukaa kimya pale wanapofanyiwa vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.
Alisema uelewa wa jamii juu ya haki zao bado ni changamoto huku umaskini ukiendelea kuwa kisingizio cha manyanyaso hayo hasa katika jamii ya vijijini, hivyo alidai ni wajibu kwa Serikali kuhakikisha inawajengea uwezo wakazi hao pamoja na kujenga miundombinu ya kutosha ili kuondoa kero zinazosababisha uduni wa maisha ambao hutumika kama kigezo cha kuendelea kuwepo kwa tatizo hili," alisema.
Awali alisema utafiti huo pia umebaini kuendelea kuwepo kwa ndoa za utotoni hivyo ni vyema sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ikafanyiwa marekebisho kwa lengo la kuzuia kuolewa msichana aliye chini ya umri wa miaka 18. Uzinduzi wa ripoti hiyo ni mwendelezo wa utekelezaji wa mradi wa kujenga na kuimarisha usawa wa kijinsia na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (GEWEII) unaoshirikisha mashirika yanayotetea haki za jamii hasa wananwake na watoto yakiwemo TAMWA, Jumuiya Wanawake Wanasheria Zanzibar (ZAFELA), Chama cha Wanasheria Wananwake (TUWLA), Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na Kituo cha Usuluhishi cha TAMWA (CRC

No comments:

Post a Comment